Sibuka FM

Makarani 792  wa Uchaguzi Maswa wapewa Somo

25 October 2025, 3:16 pm

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Maswa mashariki na Maswa Magharibi akizungumza wakati wa Ufunguzi wa mafunzo kwa Makarani waongozaji wa kupiga kura leo Oktoba 25, 2025 Picha na Nicholaus Machunda

Makarani  waongozaji  wapiga  Kura  katika  Jimbo la  Maswa  Mashariki na Jimbo la  Maswa Magharibi wameaswa  kuzingatia  Kanuni, Miongozo  na  Sheria  za  Uchaguzi   zilizotolewa na Tume Huru ya  Taifa ya Uchaguzi  ili kuepuka  migogoro isiyokuwa ya lazima

Nasaha  hizo zimetolewa  na  Msimizi  wa Uchaguzi  Jimbo la  Maswa Mashariki na  Maswa  Magharibi  Ndugu Julius  Ikongora  John  leo  Oktoba 25, 2025  wakati wa  Ufunguzi  wa  Mafunzo  ya  siku moja  kwa  Makarani  waongozaji  yaliyofanyika  katika Ukumbi wa  Msechu  Wilayani  hapa

sauti ya Julius Ikongora John Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Maswa mashariki na Maswa Magharibi

Ndugu  Ikongora  ameongeza  kuwa  uteuzi wa  Makarani  hao  umezingatia   kifungu cha  76 cha  Sheria  ya  Uchaguzi  wa Rais, Wabunge  na Madiwani   Namba 1 wa Mwaka 2025 , hivyo wana wajibu wa kutekeleza majukumu ya Uchaguzi  kwa  niaba  ya  Tume

sauti ya Julius Ikongora John Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Maswa mashariki na Maswa Magharibi
Msimamizi msaidizi wa uchaguzi jimbo la Maswa mashariki na maswa mgharibi ndugu Masanja Kengese akizungumza wakati wa mafunzo

Awali akitoa  ufafanuzi  kwa  Makarani  waongozaji  juu  ya Sheria  za  Uchaguzi ,  Msimamizi  msaidizi  wa   Uchaguzi  ngazi ya  Wilayani   ndugu  Masanja Kengese amewataka  Makarani   hao kuviishi  viapo  vyao  wakati  wote  wa  utekelezaji  wa  shughuli za  Uchaguzi.

sauti ya Masanja Kengese msimamizi msaidizi Jimbo la maswa mashariki na Maswa magharibi

Nao  baadhi ya  Makarani  waongozaji  wa  Uchaguzi  wamezungumzia  namna walivyojiandaa kutekeleza  majukumu yao  pamoja  na  kutoa  vipaumbele  kwa  makundi  maalumu  ikiwemo  wazee, watu wenye  ulemavu na akina mama wajawazito  na  wanaonyonyesha

sauti za baadhi ya makarani waongozaji wa kupiga kura