Sibuka FM
Sibuka FM
27 August 2025, 11:23 pm

Maswa imekuwa nyuma kimaendeleo kuna mambo hayako sawa ikiwemo suala la changamoto ya zao la pamba ambalo ndio zao kuu la biashara kwa mkoa wetu wa Simiyu lakini inashangaza Bei inaendelea Kushuka kila msimu na wakulima kukopwa pamba yao hivyo nitaenda kuboresha changamoto hiyo ” Dkt George Lugomela “
Mgombe Ubunge Jimbo la Maswa Mashariki kupitia chama cha Mapinduzi ccm Dkt George Lugomela amerejesha fomu ya uteuzi wa kugombea nafasi hiyo huku akitaja vipaumbele vyake ni maji, elimu, afya pamoja kushughulikia changamoto za zao la Pamba ili lilete tija kwa wakulima.
Dkt Lugomela amesema kuwa anawashukuru wote waliompigia kura na wale ambao hawakumpigia katika mchakato wa kura za maoni kwani alikuwa na ndoto ya muda mrefu ya kuwatumikia wana Maswa kupitia nafasi ya Ubunge na kuahidi kuwa mbunge wa watu wote.

Kwa upande wake katibu wa ccm Mkoa wa Simiyu ndugu Eva Michael Degeleki amewataka wanachama wa chama hicho kuvunja makundi na kuwa na kundi moja litakalofanikisha ushindi katika uchaguzi mkuu ngazi za madiwani, wabunge na Rais


