Sibuka FM

Bodaboda Maswa wakiri kutozijua sheria za barabarani

14 June 2025, 10:09 am

Mkuu wa Wilaya Maswa Dkt Vicent Anney akizungumza na maafisa usafirishaji wilayani Maswa. Picha na Nicholaus Machunda

Imebainishwa kuwa ongezeko la ajali za barabarani wilayani Maswa mkoani Simiyu,umetajwa kusababishwa na waendesha bodaboda wasiojua sheria za usalama barabarani hali iliyomlazimu mkuu wa Wilaya hiyo kukutana na bodaboda hao.

Na Alex Sayi

Baadhi ya waendesha bodaboda wilayani Maswa mkoani Simiyu walia na elimu za usalama barabani kwa madai ya marejesho kwa mabosi wao yanawafanya  wafukuzane na muda hali inayowapelekea wasizingatie sheria na alama za barabarani

Sauti za watoa huduma ya usafirishaji Maswa

        Akizungumza na bodaboda hao  Mkuu wa  Wilaya  ya  Maswa  mkoa  wa  Simiyu  Dkt  Vicent  Naano  Anney  amewataka  maafisa  Usafirishaji  hao  kuhakikisha  wanashirikiana na Jeshi la polisi nakuwahimiza kuunda vikundi ili waweze kukopeshwa Pikipiki

Sauti ya Mkuu wa Wilaya Maswa Dkt,Vicent Anney

Aidha Mkuu  wa  Usalama  barabarani  wilayani  hapa, Mkaguzi  Msaidizi  wa  Polisi  James  Nyorobi amewataka  waendesha  boda boda  kuzingatia  sheria  za  barabarani ikiwemo  kuvaa  kofia  ngumu, na  kuzingatia matumizi  ya  taa  za  kuongozea  magari

(DTO) Wilaya ya Maswa Mkaguzi Msaidizi wa Polisi James Nyorobi.Picha na Nicholaus Machunda
Sauti ya (DTO)Mkaguzi Msaidizi wa Polisi James Nyorobi