Sibuka FM

Wananchi Maswa watoa kilio kwa DC  Anney

22 May 2025, 2:02 pm

Picha aliyeshika Mic ni Mhe, Dkt Vicent Anney Mkuu wa Wilaya ya Maswa akizungumza na wananchi wa kata ya Dakama katika Mkutano wa hadhara. Picha na Nicholaus Machunda

Migogoro mingi ya Wanandoa inasababishwa na kutokuandika Wosia inapotokea mume amefariki Dunia ndugu wa mwanaume wanakuja juu na kumdhurumu mali mjane aliyeachwa na marehemu wakati mali hizo wamezitafuta wawili hao. ” Dc Dkt Vicent Anney “

Wananchi  wa  kata  za  Sangamwalugesha, Dakama  na  Lalago  zilizopo  Wilaya  ya  Maswa  Mkoa  wa  Simiyu  wameshindwa   kujizuia  na  kutoa  kero  zao  kwa  Mkuu  wa  Wilaya  hiyo  wakati  wa  Mkutano  wa  hadhara  wenye  lengo  la  kusikiliza  kero  mbalimbali za  Wananchi

Wananchi  hao  wameeleza  kuwa  kumekuwepo  na  changamoto  za  soko,  Mirathi  na  Upimaji  wa  ardhi  katika  maeneo  yao  hivyo  wakamuomba  Mkuu  wa  wilaya  azishughulikie  changamoto  hizo  ili  wananchi  waendelee  kuwa  na  imani  na  Serikali  yao

sauti za baadhi ya wananchi waliotoa kero zao kwa Mkuu wa Wilaya

Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  Ndugu  Maisha  Mtipa  na   Rukia Saidi kutoka  Mama Samia Legal  Aid   wakatoa  Ufafanuzi na kuwaondolea  hofu  wananchi  wa Sangamwalugesha, Dakama  na  Lalago  kuhusu  Masuala  ya kuanzisha  Soko, Msaada  wa  kisheria  na Migogoro  ya  Ardhi

Sauti Rukia Saidi na DED Maswa Maisha Mtipa wakitoa majibu kwa Wananchi

Kisha  Mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa  Mhe  Dkt   Vicent  Naano  Anney  akatoa  maagizo  ya  Serikali  kuhusu  changamoto  zilizowasilishwa  na  Wananchi  ikiwepo  kupeleka  Umeme  katika  shule  ya  Msingi   Mwanindo  ifikapo  Augost  30,  2025

sauti ya Dc Anney akitoa maagizo ya Serikali kuhusu kero zilizoulizwa na wananchi
Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Anney akizungumza na Wananchi wa Kata ya Sangamwalugesha
Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Anney akizungumza na Wananchi wa Kata ya Lalago