Sibuka FM

DC Gidarya awafunda CWT Maswa, awataka wasitengenezeane ‘ajali’

20 March 2025, 12:21 pm

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe, Anna Gidarya akiongea na Wajumbe wakati wa Uchaguzi wa Vingozi wa CWT Wilaya Maswa. Picha na Nichlaus Machunda

Nendeni mkasimamie haki na Stahiki za walimu wenzenu huko vijijini, kuna walimu wengi wananyanyasika na kudhurumiwa haki zao nyie viongozi mkawe chachu na siyo kikwazo na Kuwanyanyasa wenzenu walio chini yenu. ” Dc Anna Gidarya”

Kaimu  Mkuu  wa  Wilaya ya  Maswa   Mhe  Anna  Gidarya  ambaye  ni  Mkuu  wa  Wilaya  ya  Itilima   Mkoani  Simiyu   amewata  viongozi   wa  Chama  cha  Walimu  Tanzania   CWT  Wilaya  ya  Maswa   waliochaguliwa  kuhakikisha wanaenda  kutatua  changamoto  za   Walimu  hasa  maeneo  ya  pembezoni  mwa  Mji.

Mhe,  Gidarya  amesema  hayo  alipokuwa  Mgeni  rasmi  katika Uchaguzi  wa  Viongozi  wa  cwt   Maswa  na  kusema  kuwa  walimu  wanachangamoto  nyingi  sana  huko   vijijini  zinazohitaji  kutatuliwa  na  zingine  kufikishwa  mamlaka  za  juu  zaidi  ili kutafutiwa  ufumbuzi  na  siyo  kwenda  kuwanyanya  na  kujifanya  Mungu  watu.

Sauti ya Mhe, Anna Gidarya katika Uchaguzi wa CWT Maswa

Mhe  Gidarya  ameongeza  kuwa  cwt  malengo  yake  makubwa  ni  pamoja na    Kusimamia  na  kutetea  haki   za  walimu   hivyo  viongozi   waliopatikana   wakasimamie  Masilahi  ya  walimu  na  kuwa  na  Umoja  katika  kazi  zao  huku  akiwataka  kuzisoma  sheria  za  Utumishi  wa  Umma  na  kuzielewa ili  kuepuka  migogoro  na  waajiri   wao.

Sauti ya Anna Gidarya kuhusu kwenda kudumisha upendo na kutetea haki za walimu
Baadhi ya Viongozi wa cwt maswa waliochaguliwa, wa kwanza mwenye miwani ni Zacharia Munubi( mwenyekiti) akifuatiwa na Chesta Kombe mwenye kaunda suti ( Mweka Hazina ),wa tatu waliokaa ni Devotha Soko Mwakilishi kundi la wanake na viongozi wengi

 Akitangaza  matokeo  ya  Uchaguzi  wa  Viongozi   wa  nafasi  mbalimbali  katika  Chama  hicho,  Katibu   wa   cwt  Mkoa  wa  Simiyu  Lucy  Masengenya   amesema  katika  nafasi  ya  Mwenyekiti  aliyechaguliwa ni   Zacharia  s. Munubi   kwa  kura   153  kati ya  kura  186  zilizopigwa  akiwashinda   Eliud  k. John aliyepata  kura  14, akifuatiwa na Mathew  Kamalamo  aliyepata  kura  10,  nafasi ya  nne  ni  Ally Sadi  alipata  kura  4, nafasi ya  tano  ni  Joseph  Shabenesho  kura  3 huku  nafasi  ya  mwisho  wakigongana  wawili  Silvester  Butabu  Edward  na  Godi   Kiduma  waliopata  kura  1

sauti ya Lucy Masegenya akitangaza matokeo ya Uchaguzi cwt Maswa

Katika  nafasi  ya  mweka  hazina  cwt  Maswa  alichaguliwa   Chesta   Kombe  kwa  kura  147 akifuatiwa na   Lesta  Lucas (12),  Moses  Lameshi (9), Saguda  Kulwa (8)  na  Taraba  b. taraba  (5)   huku  kundi  la  Uwakilishi  ( KE )   akishinda    Devotha   Soko  aliyepata  kura   93 akifuatiwa  na  Advelah  Kashenya aliyepata  kura  71  na  Chiku  Mohamed  akipata  kura  22.

sauti ya Lucy Masegenya akitangaza matokeo ya Uchaguzi cwt Maswa

Baada  ya  Uchaguzi  mwenyekiti   aliyechaguliwa  akawashukuru  wajumbe  wote  wa  Mkutano  kwa  kumchagua   tena  kwa  mara  nyingi  ili  aendelee  kuwatukia na  kuwaahidi  kuendeleza  alipoishia  huku  akiwaomba  ushirikiano  katika  kutimiza  Majukumu  yake.

Zacharia Munubi akitoa neno la shukurani baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa cwt Wilaya ya Maswa