Sibuka FM

RC Kihongosi: Chagueni viongozi  wenye sifa uchaguzi serikali za mitaa

29 September 2024, 10:16 am

Pichani aliyesimama ( ameshika mic) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mh Kenan Laban Kihongosi akiwa katika Mkutano wa hadhara Kata ya Bugalama Wilayani Maswa wakati wa Kusikiliza kero za Wananchi na kuzitafutia Utatuzi. Picha na Nicholaus Machunda

Niwaombe sana wananchi wa Maswa msikubali kuhamasishwa na watu wenye nia ovu ya kuvuruga na uchochezi ili kuharibu amani kwani amani ikipotea wa kwanza kuumia ni watoto, akina mama na wazee.

Mkuu  wa  Mkoa   wa  Simiyu  Mh  Kenani  Laban  Kihongosi amewataka  wananchi  kuchagua  Viongozi   wenye  Sifa  za  kuwaongoza  na  siyo  kuchagua  kwa Ushabiki na  Upendeleo maana  ndio  wataoenda  kuwatetea  katika  maamuzi  ya  ngazi  za juu.

Mkuu  wa   Mkoa  ametoa  nasaha  hizo  kwa  nyakati tofauti  katika  Mikutano  yake  ya  hadhara  Wilayani  Maswa  yenye lengo  la  Kusikiliza  Kero  za  Wananchi  na  kuzitafutia  Ufumbuzi  ili Wananchi    waendelee   kuiamini   Serikali  yao.

Hii hapa Sauti ya RC Kihongosi kuhusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

RC  Kihongosi  ameongeza  kuwa   wananchi  wasikubali  kutumiwa  na   baadhi  ya  Wanasiasa  ili  kuvuruga  Amani  tuliyonayo  kwa  ajili  ya  Manufaa  ya   Watu   Wachache  ambao  hawana  Nia  nzuri  huku akitoleA  ufafanuzi Suala  la  Watu  kutekwa  na  Kutolewa  Figo

Sauti ya RC Kihongosi – tahadhari kuhusu Uvunjifu wa amani

Katika  mkutano  huo  suala  la  changamoto  ya  Maji  kuuziwa   shilingi 50  hadi  60  kwa  ndoo  ya  Lita  20  badala  ya  shilingi  40   likaibuliwa  na  Wananchi  ambapo  Mkurugenzi  wa  Mamlaka  ya  Maji  na  Usafi  wa  Mazingira  Maswa  (MAUWASA     Mhandisi  Nandi  Mathias  akatoa  Ufafanuzi.

Sauti ya Nandi Mathias (MAUWASA ) ufafanuzi kuhusu Maji Mwabayanda

Baada  ya  Ufafanuzi  huo  Mkuu  wa  Mkoa  wa  Simiyu  Mh  Kihongosi  akatoa  maagizo  hukusu  Wananchi  kupandishiwa  gharama  za  Maji  kiholela  huku  akiwataka  waliopewa  dhamana  ya  kuuza  Maji  kutowanyanyasa  Wananchi  kwa  Kigezo  cha  Sungusungu

sauti ya RC Kihongosi akitoa maagizo kwa MAUWASA

Mkuu  wa  Mkoa   yupo  katika  Ziara  ya  Siku  Sita  kuanzia  26  Sept  hadi 01  Oct,  2024  Wilayani  Maswa  kwa  ajili  ya  kusikiliza  Kero  za  Wananchi  na  kuzitafutia  Ufumbuzi  na  zingine  kuzibeba  kwa  ajili  ya  Ufuatiliaji  Zaidi

Wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mh Kihongosi ambaye hayupo Pichani
Wananchi wakiuliza Maswa kwa Mkuu wa Mkoa katika Mkutano wa hadhara