Sibuka FM

RC Kihongosi aonya wanaotoa taarifa za   taharuki kwa jamii

27 September 2024, 8:49 pm

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu (aliyesimama Mbele) Mhe Kenan Kihongosi akizungumza na Wananchi wakati wa kusikiliza Kero na Kuzitafutia Ufumbuzi katika Ziara yake Wilayani Maswa. Picha na Nicholaus Machunda

Wananchi wilayani Maswa zipuuzeni taarifa za watoto kutekwa na kutolewa figo, hao ni wapotoshaji tu wenye lengo la kuondoa amani ya taifa letu.

Mkuu  wa  Mkoa  wa  Simiyu  Mh  Kenani  Laban  Kihongosi   ameonya  watu  wanaoeneza  taarifa  za  Taharuki  za  Watoto  kupotea,,  kutekwa  na  Wengine  kutolewa   Figo..

Onyo  hilo amelitoa   kwa  Nyakati  Tofauti   katika  Mikutano yake  ya  Hadhara  yenye  lengo  la  kusikiliza  kero  za  Wananchi  na  Kuzitafutia  Ufumbuzi  katika  Kata  za Dakama, Sangamwalugesha, Lalago  na  Mbaragane zilizopo  Wilayani  Maswa.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu wakati akisikiliza kero za Wananchi wa Maswa

Mhe, Kihongosi  amesema  kumekuwepo  na taarifa  za  Taharuki  kwa  Jamii  kuhusu  watu  kutolewa  Figo, Kutekwa  na  Watoto  kupotea  kitu  ambacho  siyo  kweli  kwani  hamna  hata  mmoja  aliyedhibitisha  mtoto  wake  kutekwa    na  amewataka  kulinda na kudumisha amani  ya  Nchi  yetu.

Sauti ya RC Kihongosi akitoa Ufafanuzi wa taaruki ya watu kuuliwa na kutolewa Figo

Katika  Ziara  hiyo  ya  Mh  Mkuu  wa  Mkoa , Wananchi  walipata  nafasi  ya  kuwasilisha  Kero  zao zinazowasumbua  ikiwemo  changamoto  za  Umeme, Barabara  na  Uhaba  wa  Watumishi katika  Zahanati  na Shule  za  Msingi  na  Sekondari

Pichani ni baadhi wa Wananchi wakiuliza Maswali kwa RC Kihongosi
Sauti za Wananchi Maswa wakitoa Changamoto zao kwa RC Kenan Kihongosi

Meneja  Tanesco  Mkoa  wa  Simiyu   Alistidia  Clemence Kashemeza  na  Mkuu  wa  Division  ya Elimu  Msingi  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  Dkt   Lucy  Kulong’wa   wakatoa  Majibu  ya  Serikali  kuhusu  Changamoto  hizo.

Sauti ya Wataalamu wakitoa Majibu kwa Wananchi kuhusu changamoto zilizoulizwa
Pichani ni mkuu wa Division ya Elimu Msingi Maswa Dkt Lucy Kulong’wa akitoa Ufafanuzi kwa Wananchi