Sibuka FM

Mpina agawa vifaa vya TEHAMA jimboni

13 August 2024, 10:47 pm

Pichani aliyevaa Miwani na Skafu ni Mhe Luhaga Mpina Mbunge wa Jimbo la Kisesa akikabidhi Vifaa vya TEHAMA ( Komputa na Photocopy Mashine ) Katika Shule za Sekondari tisa vyenye thamani ya Mil 22. 5 ili Kusaidia Kuongeza Ufaulu kwa Wanafunzi. Picha na Nicholaus Machunda

Nicholaus Machunda – Simiyu

Mbunge  wa  Jimbo  la  Kisesa  lililopo  wilayani  Meatu  mkoani  Simiyu  Mhe. Luhaga  Joelson  Mpina  amekabidhi  vifaa  vya   TEHAMA  katika  shule  tisa  za  Sekondari jimboni  kwake  vyenye  thamani ya  Shilingi  Milioni  22. 5  ili  kusaidia  Utendaji  kazi  na  Kuongeza  Ufaulu.

Akikabidhi  Vifaa  hivyo  vya  TEHAMA   ikiwemo  Mashine  ya  Kudurufu  Karatasi (Photocopy  Mashine ) na  Komputa  kwa  ajili  ya  kusaidia  Uandaaji  wa  Majaribio  ya  Mitihani  kwa  Wanafunzi  na  shughuli  mbalimbali  za  Kiofisi huku akitaja gharama za kila kifaa

Hii hapa ni Sauti ya Luhaga Mpina wakati wa kukabidhi vifaa vya TEHAMA

Aidha  Mhe  Mpina  ametatua  Changamoto  ya  Uhaba  wa  Matundu  ya  vyoo  na Mfumo  wa  Umeme  katika  Shule  ya  Sekondari  Mwakaluba  baada  ya  kuelezwa  kuwa  shule  hiyo  ina uhaba  wa  Matundu  ya  Vyoo  kwa  Wanafunzi  huku   Walimu  wakichangia  Matundu  hayo na  Wanafunzi

Hii hapa sauti ya Luhaga Mpina kuhusu changamoto ya matundu ya vyoo

Akimkaribisha  Mgeni  rasmi  katika  hafla  hiyo, Kaimu  Afisa  Elimu  Sekondari  Wilaya  ya  Meatu  Mwl  Antony Luyeye  amesema  kuwa   Mhe  Mpina  amekuwa  akijitoa  sana  katika  kusaidia  Idara  ya  Elimu  hivyo  wanampongeza  na Kumshukuru sana

Sauti ya Mwl Antony Luyeye Kaimu afisa Elimu Sekondari Mweatu

Akitoa  taarifa  fupi  kwa  Mgeni  rasmi,   Makamu  Mkuu  wa  Shule  ya  Sekondari  Mwakaluba  Mwalimu  Woga  Obadi  Charles  amesema   kuwa changamoto  kubwa  katika shule hiyo ni  Uhaba  wa  Matundu  ya  vyoo  baada  ya  kutitia  vile  vya  awali  kutokana  na  Mvua  kubwa  zilizokuwa  zikinyesha .

Sauti ya Makamu mkuu wa Shule ya Sekondari Mwakaluba Mwl Woga Charles
Mashine ya kudurufu karatasi ni miongoni mwa Vifaa vilivyokabidhiwa na Mbunge

Mwalimu   Makinga  Bulenya   ni  Mkuu  wa  Shule  ya  Sekondari  Kisesa  ambapo  ni  Miongoni  mwa  shule   Tisa  zilizopata  Vifaa   vya  TEHAMA   amemshukuru   Mbunge  wa  Jimbo  la  Kisesa  Mhe,  Luhaga  Mpina  kwa  Ushirikiano  anaotoa  katika  Kuinua  Elimu  Jimboni  hapo.

Sauti ya Mkuu wa Shule ya Sekondari Kisesa Mwl Makinga Bulenya

Nao  baadhi  ya  Wanafunzi  waliozungumza  na  RADIO  SIBUKA  FM   wamemshukuru  Mbunge  wao  kwa  kuleta  Vifaa  hivyo  vya  TEHAMA  na  kumuahidi  kufanya  vizuri  katika  Mitihani  yao  na  Kuongeza  Ufaulu

S auti za baadhi ya wanafunzi wakimshukuru Mbunge wao Mhe Luhaga Mpina
Wanafunzi wa shule ya Sekondari Mwakaluba
Mbunge wa Jimbo la Kisesa akifurahia Jambo na wanafunzi wa Kisesa Sec