Sibuka FM

Wanafunzi mabalozi wazuri wa usalama barabarani Bariadi

18 March 2025, 9:20 pm

Mabalozi wa usalama barabarani mkoa wa Simiyu wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Sima B wakati wakitoa elimu ya usalama barabarani Picha na Anitha Balingilaki

Elimu ya usalama barabarani bado haikwepeki hivyo mamlaka husika zinao wajibu wa kutoa elimu hasa kwa makundi ambayo yanaweza kuwa msaada mkubwa wa kufikisha elimu kwa jamii kubwa”.

Na, Daniel Manyanga 

Katika kuhakikisha ajali za barabarani zinaisha au kupungua mkoani Simiyu Wanafunzi wametajwa kuwa mabalozi wazuri wa utoaji wa taarifa za usalama barabarani  kwenye jamii inayowazunguka hali inayotajwa kuwa njia bora ya kuifikia idadi kubwa ya wananchi Ili kumaliza ajali hizo.

Mwenyekiti wa RSA mkoa wa Simiyu,Manjale Magembe akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Sima B wakati wa utoaji elimu ya usalama barabarani Picha na Anitha Balingilaki

Wakizungumza na Sibuka fm wakati wa utoaji elimu hiyo kwa wanafunzi wa shule ya msingi Sima B mjini Bariadi,Manjale Magembe ambaye ni mwenyekiti wa RSA mkoa na Alchangela Kashemeza katibu wa RSA mkoa huo  wamesema lengo la utoaji elimu ya usalama barabarani katika kundi hilo ni kutanua wigo wa elimu kwa jamii ili kuweza kumaliza changamoto za ajali barabarani.

Sauti za viongozi mabalozi wa usalama barabarani wakizungumza namna ambavyo elimu hii itasaidia kumaliza ajali ambazo siyo za lazima
Katibu wa RSA mkoa wa Simiyu, Alchangela Kashemeza akizungumza na wanafunzi wakati wa utoaji elimu ya usalama barabarani Picha na Anitha Balingilaki

CPL,Lutego Buswelu ni askari wa usalama barabarani wilayani Bariadi amesema kuna kila sababu ya kila mtumiaji wa barabara kizingatia sheria za usalama wa barabarani katika kumaliza ajali ambazo siyo za lazima

Sautia ya CPL,Lutego askari wa usalama barabarani wilayani Bariadi akizungumzia umuhimu wa elimu hiyo hasa kwa kundi la wanafunzi
Muonekano wa picha ya pamoja ya viongozi mabalozi wa usalama barabarani na maafisa usafirishaji wakiendelea kutoa elimu ya usalama barabarani

Wakiongea kwa niaba ya wanafunzi ,Isaka Mauna na Felister Daniel  wamesema kuwa ujio wa elimu hiyo utasaidia kupunguza ajali za barabarani kwa kuwa wamejuwa baadhi ya alama muhimu za usalama barabarani.

Sauti ya wanafunzi wa shule ya msingi Sima B wakizungumza namna ambavyo elimu hiyo itawasaidia katika kumaliza ajali za barabarani ambazo siyo za lazima