Sibuka FM

Madereva wa magari madogo ya abiria wagoma kufanya usafirishaji Bariadi

12 March 2025, 6:07 pm

Muonekano wa picha za magari madogo yakiwa yamepaki katika ofisi za chama cha mapinduzi ccm mkoa wa Simiyu Picha kutoka maktaba ya Sibuka fm

Hoja za madereva wa daladala mkoa wa Simiyu naomba zisikilizwe maana kuna hoja kubwa sana ni kweli serikali yangu ya jamhuri ya muungano wa Tanzania imejenga stund tena nzuri kweli ya kisasa lakini sasa hatuwezi kuwachanganya hawa tunaenda kuua biashara yao naomba busara zitumike katika kushughulikia hili maana Kambare ni mkubwa hivyo chakula chake ni dagaa wadogo”.

Na, Daniel Manyanga

Madereva wanaoendesha magari madogo ya abiria mkoani Simiyu wamegoma kwa siku mbili mfululizo kufanya safari lengo likiwa kuishinikiza serikali kuwatengea eneo la kupakia abiria tofauti na sasa ambapo wanatakiwa kupakia stand kuu ya mabasi hali ambayo imetajwa kuwanyima riziki mkoani hapo.

Akizungumza na Sibuka fm makamu mwenyekiti wa umoja wa daladala mkoa wa Simiyu,Mussa Pomokela amesema kupakia stund kuu ya mabasi ya mkoa ni kuwanyima riziki za wao kupata abiria kutokana kuwepo kwa mabasi mengi makubwa yanayofanya safari kuanzia hapo hapo stund hivyo ngumu kwa abiria kupanda gari ndogo.

Sauti ya makamu mwenyekiti wa umoja wa daladala na baadhi ya madereva wakijenga za kwanini hawataki kwenda kupakia abiria stund kuu ya mabasi

Akijibu malalamiko hayo mkuu wilaya ya Bariadi, Simon Simalenga amesema ni vema madereva hao wakafuata sheria zilizopo na siyo serikali ya wilaya ifate kile wao wanachokitaka maana tayari serikali ya imeshajenga stund ya mabasi ya mkoa na kuna eneo la kupakia kwa magari hayo madogo.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Bariadi, Simon Simalenga akizungumza na madereva wa daladala baada ya mgomo wa kufanya kazi ya kusafirisha

Simon Simalenga kuhusu baadhi ya magari kukamatwa ametoa maagizo kwa mamlaka zilizohusika kukamata magari hayo kuyaachia mara Moja magari yaweze kurudi kwa wenye nayo.

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Bariadi akitoa ufafanuzi wa mgomo huo na sababu za magari baadhi kukamatwa na mamlaka husika