Sibuka FM

DC Maswa asisitiza ushirikiano kwa watumishi wa umma

26 February 2025, 11:46 am

Pichani:Mkuu Mpya wa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu Dkt,Vincent Anney akitoa neno mara baada yakukabidhiwa ofisi kwenye Makabidhiano yaliyofanyika Februari,25/2025.Picha na Paul Yahana

DC mpya Wilayani Maswa Mkoani Simiyu awataka watumishi na watendaji kutafsiri maono ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwa vitendo,hali itakayoisaidia Wilaya hiyo kupiga hatua za kimaendeleo.

Na,Paul Yohana-Maswa-Simiyu

Mkuu mpya wa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu Dkt,Vincent Anney amewaomba watumishi wa taasisi mbalimbali na wajumbe wa kamati ya ulinzi na Usalama Wilayani hapa kufanya kazi kwa ushirikiano ili kufikisha maendeleo kwa wananchi.

 hayo yamesemwa na Dkt,Anney mara baada ya kukabidhiwa ofisi na aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya  Maswa Mh,Aswege Kaminyoge.

Sauti ya Mkuu Mpya wa Wilaya ya Maswa Dkt,Vincent Anney

Aidha  Dkt.Anney amehimiza kufanya kazi kama timu na mtumishi yeyote akiona jambo lolote ambalo linahusu wilaya ya Maswa asisite kutoa taarifa mapema ili kufikia ndoto ya Rais wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hasan ya kufikisha maendelo kwa jamii

Sauti ya Mkuu Mpya wa Wilaya ya Maswa Dkt,Vincent Anney

Kwa upande wake  aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Maswa Mh.Aswege Kaminyoge ambae kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mkoani Mara akitoa taarifa kwa mkuu mpya wa Wilaya ya Maswa Dkt, Anney amesema kuwa Wilaya ya Maswa imetekeleza miradi mingi ndani ya kipindi cha miaka (4)ya utawala wa Dkt,Samia.

Sauti ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mh,Aswege Kaminyoge
Pichani:Wa kwanza kulia mwenye Suti ya Kijivu ni Mkuu Mpya wa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu,Dkt,Vincent Anney akifuatiwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Maswa Mkoani hapa,Bw,Athuman Kalaghe wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya watumishi na wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya wakati wa makabidhiano ya Ofisi,Feb,25/2025.Picha na Paul Yohana.