Sibuka FM

DC mpya Maswa atoa angalizo kwa watumishi wazembe

26 February 2025, 10:34 am

Pichani:Kushoto mwenye Suti ya Kijivu ni Mkuu mpya wa Wilaya ya Maswa Dkt,Vincent Anney akikabidhiwa nyaraka za Ofisi hiyo na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo aliyehamishiwa Wilaya ya Bunda Mkoani Mara Mh,Aswege Kaminyoge mwenye Suti nyeusi,makabidhiano yaliyofanyika Februari,25/2025.Picha na Neema Solo

Watumishi wilayani Maswa mkoani Simiyu wakumbushwa kuwajibika kwa weledi ili kuendana na kasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Na,Alex Sayi-Maswa Simiyu

Mkuu mpya wa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu Dkt, Vincent Anney amewakumbusha watumishi Wilayani hapa kuhakikisha wanawajibika kikamilifu ili kuwasogezea maendeleo wananchi.

hayo yamesemwa na Dkt,Anney mara baada yakukabidhiwa ofisi hiyo na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Mh,Aswege Kaminyoge aliyehamishiwa kituo Kipya cha kazi Wilaya ya Bunda Mkoani Mara,kufuatia mabadiriko madogo yaliyofanywa na Rais Samia Februari,21/2025

Awali Dkt,Anney akizungumza kwenye makabidhiano hayo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt,Samia Suluhu Hasani kwakuendelea kumwamini kwenye majukumu hayo ya ukuu wa Wilaya,huku akibainisha kuwa kwenye utumishi wake siyo muumini wa utendaji kazi wa michakato

Sauti ya Mkuu mpya wa Wilaya ya Maswa Dkt,Vincent Anney

Kwa upande wake aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Maswa Aswege Kaminyoge amemshukuru Rais Samia kwakumwamini kuendelea na majukumu yake ya ukuu wa Wilaya

Sauti ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mh,Aswege Kaminyoge

Aidha kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Maswa Athuman Kalaghe akishukuru kwa niaba ya watumishi wa ofisi hiyo alimtakia kilalakheri aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Maswa,Mh,Aswege Kaminyoge(a.k.a,Professor )                                                          

Sauti ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Maswa Bw,Athuman Kalaghe
Pichani:Wajumbe wa kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya ya Maswa,pamoja na baadhi ya watumishi na wakuu wa taasisi Wilayani hapa wakiwa kwenye picha ya pamoja kwenye shughuli ya makabidhiano ya ofisi baina ya Dkt,Vincent Anney na Mh,Aswege Kaminyoge.Picha na Neema Solo.