Sibuka FM

Maswa mbioni kuzalisha chaki zitakazouzwa nchi nzima

25 February 2025, 6:17 pm

Pichani: Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya,Maswa Bw, Maisha Mtipa akitoa ufafanuzi kwa Naibu waziri wa Viwanda na Biashara Mh,Exaud Kigahe alipotembelea na kugagua utendaji kazi wa kiwanda cha kuzalisha Chaki.Picha na Neema Solo

Kiwanda cha kuzalisha chaki kilichopo wilayani Maswa mkoani Simiyu mbioni kuzalisha chaki zitakazokuwa mwarobaini kwa mahitaji ya chaki nchini kwa shule za msingi na sekondari.

Na,

Alex Sayi

Halmashauri ya Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu iko mbioni kuanza uzalishaji wa chaki zitakazouzwa Nchi nzima kwa shule za msingi na sekondari na nje ya Nchi.

Hayo yamebainishwa mbele ya  Naibu Waziri wa  Viwanda na Biashara akiwa ziarani mkoani Simiyu alipotembelea kiwanda cha kuzalisha chaki kilichopo wilayani Maswa mkoani hapa Februari 23 mwaka huu.

Akisoma taarifa ya kiwanda hicho kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halamashauri ya Wilaya ya Maswa, Afisa Mipango wa Halmashauri hiyo Bw. Julius Ikongora amesema kuwa kiwanda hicho kimegharimu zaidi ya Sh.Bil.10

Sauti ya Afisa Mipango Wilaya ya Maswa Bw,Julius Ikongora
Pichani: Afisa Mipango wa Wilaya ya Maswa,Bw,Julius Ikongora akisoma taarifa ya kiwanda kwa Naibu waziri wa Viwanda na Biasha,Mh,Exaud Kigahe alipotembelea kiwandani hapo.Picha na Neema Solo

Akizungumza na Radio Sibuka FM Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bw. Maisha Mtipa amesema kuwa anaishukuru serikali ya Mama Samia kwa kutenga fedha hizo na kubainisha kuwa kiwanda hicho kitaisaidia halmashauri hiyo kuongeza mapato yake ya ndani na kupunguza utegemezi wa mapato toka Serikali Kuu

Sauti ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ,Bw,Maisha Mtipa

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh,Exaud Kigahe ameipongeza Halmashauri hiyo kwa uamuzi wake wa kujiendesha kibiashara kupitia kampuni tanzu ya Ng’hami Industrial Kampani

Sauti ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh,Exaud Kigahe
Pichani:Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa,Bw,Maisha Mtipa,akifuatiwa na kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi,Mh,Saimon Simalenga akifuatiwa na Naibu waziri wa Viwanda na Biashara Mh,Exaud Kigahe wa mwisho kulia ni katibu tawala Mkoa wa Simiyu, Bi,Prisca Kayombo.Picha na Neema Solo