Sibuka FM

TRA mkoa wa Simiyu yakusanya bilioni 14.2 kwa miezi sita

24 February 2025, 3:51 pm

Kwenye picha ni meneja wa TRA mkoa wa Simiyu, Joseph Mtandika akizungumza jambo katika usiku wa tuzo wa shukrani kwa walipakodi baada ya kufanikiwa kukusanya bilioni 14.2 ndani ya miezi sita

‘‘Hakuna mtu yeyote atakayetoka nje ya nchi kuja hapa nchini kwetu kutuambia namna bora ya kulifanya taifa letu liweze kusonga mbele katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ili kufikia malengo mama ya taifa kama sisi wenyewe hatutaweza kulipa kodi kwa hiari ambapo kodi  hizo ndizo zinapeleka maendeleo kwa wananchi tulipeni kodi kwa maendeleo endelevu ya taifa hili’’.

Na,Daniel Manyanga

Mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) mkoa wa Simiyu imefanikiwa kukusanya kiasi cha fedha bilioni 14.2 kitokanacho kodi za walipakodi  katika nusu ya mwaka wa fedha 2024/25 kati ya fedha  bilioni 24.98 ambalo ni lengo katika mwaka huu wa fedha ambacho kimepangwa kukusanywa ili kusaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimkakati ya maendeleo hapa nchini.

Akizungumza katika hafra ya usiku wa shukrani kwa walipakodi ulioandaliwa na mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) meneja wa mamlaka hiyo mkoa wa Simiyu, Joseph Mtandika  amesema kuwa mkoa huo umeelekezwa kukusanya  kiasi cha fedha  bilioni 24.98 katika mwaka wa fedha 202425 lakini mpaka sasa wamefanikiwa kukusanya  zaidi ya bilioni 14 kwa kipindi cha miezi sita kutoka Julai hadi Desemba mwaka jana.

Sauti ya meneja wa TRA mkoa wa Simiyu akielezea namna ambavyo wamefanikiwa kufikia malengo ndani ya miezi sita

Kenan Kihongosi ni mkuu  wa mkoa wa Simiyu  akizungumza katika hafra ya usiku wa shukrani kwa walipakodi  amewataka walipakodi mkoani hapo kuhakikisha wanatimiza wajibu wao wa kulipa kodi kwa hiari pasipo kusubiri kushurutishwa na mamlaka husika za kikodi kwani kodi hizo husaidia kuchochea shughuli za maendeleo ikiwemo kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati hapa nchini.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Simiyu akiwataka walipakodi kulipia kwa hiari bila shuruti kutoka kwa mamlaka za kikodi
Muonekano wa mkuu wa mkoa wa Simiyu,Kenan Kihongosi akiwa kwenye moja ya shughuli Picha kutoka maktaba ya Sibuka fm

Joseph Goryo,Jackson Samuel ni  baadhi ya walipakodi waliopata tuzo za ulipakodi bora kwa hiari katika hafra hiyo wameeleza namna ambavyo  tuzo hizo zitaleta chachu ya ushindani  kwa walipakodi  huku mwakilishi wa mwenyekiti wa wafanyabiashara mkoa wa Simiyu,Boaz Ogolla ameishukuru mamalaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Simiyu kwa tuzo hizo hali ambayo inatambua umuhimu wa wafanyabiashara mkoani hapo.

Sauti ya walipakodi waliopata tuzo wakielezea namna ambavyo zitakuwa chachu za kuchochea maendeleo
Muonekano wa logo ya mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) picha kutoka maktaba ya Sibuka fm