Sibuka FM

Mnada mpya wazinduliwa Maswa, Watajwa kuongeza Mapato ya Halmashauri

2 March 2025, 11:16 am

Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Wilaya ya Maswa Robert Urassa ( aliyeshika Mic ) akitoa Ufafanuzi kwa Mgeni rasmi kuhusu utaratibu wa kufanya biashara katika Mnada huo baada ya kutembelea vizimba vya Wafanyabiashara wakati wa Uzinduzi

Malengo ya kuanzishwa kwa Mnada huo ni kusogeza huduma kwa Ukaribu ya uuzaji wa Mifugo, Upatikanaji wa Mahitaji mbalimbali ya kila siku kwa Wananchi wa Wigelekelo na maeneo jirani pamoja na kuongeza wigo wa Ukusanyaji wa Mapato katika Halmashauri

Na ; Nicholaus Machunda

Wilaya  ya  Maswa  Mkoani  Simiyu  imezindua  Mnada   Mpya  utakaosaidia  kuongeza  Mapato    ya  Halmashauri  na kusogeza  Huduma  kwa  wananchi  wa  kijiji  cha  Wigelekelo  na  Maeneo  jirani  yanayozunguka  mnada  huo.

Akizungumza wakati kuzindua  Mnada  huo  kwa niaba  ya  Mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa  Dkt  Vicent  Naano Anney, Katibu  Tawala  wa  Wilaya  hiyo  Athumani Zahoro  Kalaghe  amewapongeza  Madiwani   na  Wataalam  kwa  ubunifu  wa Mnada  huo  ambao  utaenda  kupanua  wigo  wa  huduma  kwa  wananchi na  kuongeza  mapato

sauti ya Athumani Kalaghe -DAS Maswa akizungumza wakati wa uzinduzi wa mnada wa Wigelekelo

Kalaghe ametoa  rai  kwa  wananchi wa Maswa na Maeneo jirani  kujitokeza  kuchukua  Vizimba  kwa  ajili  ya  Biashara   bure  huku  akitoa  maagizo  kwa  Mkurugenzi  kuhakikisha  wanaboresha  miundo  mbinu  katika  Mnada  huo ili iwe rafiki kwa wafanyabiashara.

sauti ya Athumani Kalaghe – DAS Maswa akizungumza wakati wa uzinduzi wa mnada
Picha aliyesimama ni Athumani Kalaghe-DAS Maswa akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mnada mpya katika kijijji cha Wigelekelo kata ya Masela, kulia ni Mhe Paul Maige mwenyekiti wa Halmashauri na kushoto ni ndugu Onesmo Makota mwenyekiti wa ccm wilaya ya Maswa

Akitoa  taarifa  kwa  Mgeni  rasmi, Mkuu  wa  Divisioni  ya  Kilimo, Mifugo  na  Uvuvi  Robert   Urassa amesema  kuwa  malengo  ya  uanzisha  mnada ni  kufikisha   kwa  ukaribu uuzaji  wa  Mifugo  pamoja na  kusogeza  huduma  kwa  Wananchi  ili  kurahisisha kupata  Mahitaji  ya  nyumbani ya  kila  siku

Sauti ya Robert Urassa – Mkuu wa Divisheni ya kilimo, mifugo na Uvuvi – Maswa

Paul  Maige   ni  Mwenyekiti  wa  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  ameeleza  mchakato  wa kuanzisha  mnada  mpya  katika  kijiji  cha  Wigelekelo  kata  ya  Masela  huku  akiwatoa  wasi wasi  wananchi  kuhusu  uwakilishi  wa  Wananchi  katika  Baraza  la  Madiwani

sauti ya Mhe Paul Maige -mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Maswa

Akitoa  salamu  za  Chama, Mwenyekiti  wa  ccm  wilaya  ya  Maswa    Onesmo  Makota  amewapongeza   wote  walioshiriki  kufanikisha   wazo   la  uanzishwaji  mnada  huo  kwani  ndio  malengo  mahususi  ya  Chama  cha  Mapinduzi  ya kusogeza  huduma  kwa  Wananchi

sauti ya Ndugu Onesmo Makota – Mwenyekiti wa ccm wilaya ya Maswa

Diwani  wa  Kata  ya  Masela  Mhe  Kulwa   Gwisu  Hinda  amesema  kuwa  aliwasilisha   kama   wazo  la   kuanzisha  mnada  kwenye  Baraza  la  Madiwani  ili  kuongeza  mapato    na  wazo  hilo  likaboreshwa  na   Wataalamu  wa  Halmashauri  na   kuanza utekelezaji hatimae kukamilika  na wananchi  kuanza  kupata  huduma  na  mahitaji  mbalimbali

sauti ya Kulwa Hinda diwani wa kata ya Masela wilayani Maswa

Baadhi  ya  Wananchi  na  Wafanya biashara  walioshiriki  Uzinduzi  wa  Mnada  Mpya  huo  wameipongeza  Halmashauri  kwa  Ubunifu  huko  wa  kusogeza  huduma   kwa  Wananchi huku  wakiomba  uboreshaji  wa  Miundo mbinu  katika   eneo  hilo  na  wananchi  waendelee  kuhamasishwa  kupeleka  biashara  zao

Baadhi ya wafanyabiashara na wananchi wakielezea furaha yao baada ya kuanzishwa kwa Mnada mpya
Pichani ni viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali walioshiriki uzinduzi wa mnada mpya wa Wigelekelo uliopo kata ya Masela wilayani Maswa