Sibuka FM

Simiyu:Chatanda viongozi wanawake tendeni haki bila kujali vyama

19 February 2025, 8:30 pm

Pichani ni Mary Chatanda akionekana akifurahia jambo wakati wa mafunzo ya matumizi ya takwimu za sensa kwa viongozi wanawake wa serikali za mitaa mkoa wa Simiyu wa chama cha mapinduzi Picha na Anitha Balingilaki

Uongozi siyo kupiga kelele ni kuleta mabadiliko chanya katika eneo lako la kiutawala kama kuna changamoto zozote zile kwa wananchi tuanataka utuambie umefanya nini kuzitatua hizo shida ili jamii iseme kweli hapa tunakiongozi na siyo msindikizaji viongozi”.

Na, Daniel Manyanga 

Mwenyekiti wa jumuiya ya umoja wa Wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT)Taifa ndugu Mary Chatanda amewataka viongozi wanawake waliochaguliwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mwaka jana mkoani Simiyu kuwatumikia wananchi  bila ubaguzi  ukiwemo wa kivyama.

Picha ni, Mary Chatanda akizungumza jambo na washiriki wa mafunzo ya matumizi ya takwimu za sensa katika kuleta usawa wa maendeleo Picha na Anitha Balingilaki

Mary Chatanda ametoa rai hiyo mapema leo hii kwenye mafunzo ya uhamasishaji wa  matumizi ya matokeo ya sensa ya mwaka 2022 kwa viongozi wanawake waliochaguliwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa katika kuleta usawa wa maendeleo kwenye maeneo husika kulingana na ukubwa wa eneo ,uhitaji wa eneo na ongezeko la watu.

Sauti ya Mary Chatanda akizungumza na viongozi wanawake wakati wa mafunzo ya matumizi ya takwimu za sensa

Akimwakilisha mtakwimu mkuu wa serikali Benedict Mugambi amesema mafunzo hayo yawasaidie viongozi hao kushiriki kikamilifu kwenye miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao ikiwemo na kukemea maswala ya rushwa.

Sauti ya Benedict Mugambi akizungumza na viongozi wanawake katika kutumia vizuri takwimu za sensa

Limi Silanga na Veronica Mabesa ni baadhi ya viongozi wanawake wa serikali za mtaa mkoani hapo wamesema kuwa mafunzo yatasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao katika maeneo ya kiutawala Ili kuleta usawa kwa wananchi.

Sauti ya viongozi wanawake mkoa wa Simiyu wakielezea namna ambavyo watayatumia mafunzo katika kuleta usawa wa maendeleo kwenye maeneo ya kiutawala
Picha ya pamoja ikiwaonyesha viongozi wanawake wakiwa wanafuatilia jambo wakati wa mafunzo Picha na Anitha Balingilaki