Sibuka FM

Wananchi jifunzeni kuhusu haki zenu za kisheria–Mahumbuga

4 February 2025, 12:00 pm

Picha ni Martha Mahumbuga Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Simiyu wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Sheria yaliyofanyika kwenye Viwanja wa Mahakama hiyo. Picha na Nicholaus Machunda

Wananchi wanapaswa Kujifunza na kuelewa haki zao za Kisheria ili waweze kushiriki kikamilifu katika Mchakato wa haki na Dira ya Maendeleo hii itajenga Uwajibikaji kwa taasisi na wadau wa kutoka Haki -“Mhe Martha Mahumbuga”

Hakimu  Mkazi  Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Simiyu Mh, Martha Johnbull Mahumbuga ametoa wito  kwa  wananchi kuwa na utamaduni wa kujifunza  haki zao za msingi ili waweze kushiriki kikamilifu katika  mchakato wa haki na maendeleo.

Wito huo umetolewa feb, 03 2025 wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria iliyofanyika katika viwanja vya mahakama hiyo wilayani bariadi mkoani simiyu.

Sauti ya Martha Mahumbuga Hakimu mahakama ya hakimu Mkazi Mkoa wa Simiyu

Akitoa salamu za Serikali Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mh, Saimon Simalenga  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mh, Kenani Kihongosi  amewapongeza kwa kufanya jukumu lao vizuri ,huku akiitaka Mahakama na wadau kuendelea kutoa elimu ili kuendelea kutambua haki zao.

Sauti ya DC Bariadi Saimon Simalenga – akitoa salamu za Serikali katika kilele cha wiki ya Sheria

Kwa upande wake mwendesha mashtaka wa serikali mkoa wa simiyu Mh, Anesius Kainunura amesema mahakama ndio chombo pekee cha utoaji wa haki, na kuongeza kuwa ili malengo makuu ya dira ya taifa ya maendeleo 2050  yaweze  kufikiwa kama  kila raia atapata haki yake ya msingi bila kikwazo. 

Sauti ya Anesius Kainunura – Mwendesha Mashitaka Mkoa wa Simiyu
Picha (aliyekatikati mstari wa mbele) Mh Martha Mahumbuga akiwa katika picha ya pamoja ya watumishi wa Mahakama katika Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu

Kwa upande wao wananchi wamesema kuwa wamependezwa nakuona kuwa uhuru wa mahakama upo lakini kuomba elimu izidi kutoolewa kwa wanawake na watoto hasa maeneo ya vijijini ambako wengi hawana elimu ya sheria.

Sauti za baadhi ya wananchi wa Mkoa wa simiyu

Kauli mbiu katika Maadhimidho hayo ya wiki ya Sheria kwa Mwaka huu 2025 ni Tanzania ya 2050 nafasi za Taasisi zinazosimamia Haki madai katika kufikia malengo makuu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo.