Chai FM

Jamii imetakiwa kusalimisha silaha haramu

23 September 2022, 5:41 am

RUNGWE-MBEYA

NA,JUDITH MWAKIBIBI

Kutokana na kampeni inayoendelea ya usalimishaji wa silaha kitaifa wananchi wilayani Rungwe mkoani Mbeya wametakiwa kusalimisha silaha haramu zinazomilikiwa kinyume na utaratibu.

Akizungumza  katika studio za radio chai FM mrakibu wa jeshi   la polisi Wilayanl ya Rungwe Sevelini Msonda amesema kuwa kila ifikapo mwezi wa tisa kunakuwa na kampeni kitaifa ya kusalimisha silaha haramu .

Aidha amesema Jeshi la Polisi Wilaya ya Rungwe limejipanga vizuri na kuhakikisha zoezi linafanyika kikamilifu na pindi kampeni ikikamilika  utaanza msako kubaini wanaomiliki  silaha kinyume na sheria.

Hata hivyo mrakibu wa jeshi la polisi  amesema mpaka sasa kwa wilaya ya Rungwe hamna mwananchi yeyote aliyesalimisha silaha hivyo ni vyema mwananchi anayemiliki silaha kinyume na utaratibu wa kisheria ajitokeze.