Sibuka FM

Maswa:wajawazito (400-450)hujifungua ndani ya  mwezi mmoja

2 March 2025, 6:38 pm

Pichani:Mwenye miwani ni mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu Dr,akipokea baadhi ya zawadi kutoka kwa kinamama waliofika Hospitalini hapo Februari,28/2025,kushoto kwake ni Bi,Caroline Shayo mwenyekiti wa umoja wa wanawake Wilaya ya Maswa na Mwenyekiti wa Mamlaka ya mji mdogo Maswa.Picha na Neema Solo.

Jamii Wilayani Maswa Mkoani Simiyu imeaswa kujenga tabia ya kuwatembelea wajawazito na wazazi wanaojifungua ili kusaidia mahitaji muhimu ya uzazi kwa wazazi hao.

Na,Alex Sayi Maswa-Simiyu

Uongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu umebainisha kuwa ndani ya mwezi mmoja hupokea wasitani wa kinamama wajawazito (400-450)

Hayo yamesemwa na mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo,Dr,Deogratius Mtaki, wakati akipokea baadhi ya zawadi zilizotolewa na umoja wa wanawake Wilayani Maswa Mkoani hapa kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Machi,08/2025.

Sauti ya Mganga Mfawidi Hospitali ya Wilaya ya Maswa,Dr,Deogratius Mtaki

kwa upande wake Afisa Maendeleo Wilaya na Mratibu wa dawati la jinsia Wilayani Maswa Mkoani hapa Bi,Basila Bruno  amesema kuwa katika kuenzi siku ya wanawake Duniani  kinamama hao kwa umoja wao wameamua kushiriki kufanya matendo ya huruma Hospitalini hapo.

Pichani:Anaezungumza ni Afisa Maendeleo Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu na Mratibu wa Dawati la Jinsia Wilaya,Bi,Basila Bruno.Picha na Neema Solo
Sauti ya Afisa Maendeleo Wilaya ya Maswa na Mratibu wa Dawati la Jinsia Wilaya,Bi,Basila Bruno

Aidha kwa upande wake mwenyekiti wa umoja wa wanawake Wilayani  Maswa Mkoani hapa na mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo Wilaya ya Maswa Bi,Caroline Shayo amesema kuwa wamefika Hospitalini hapo kutoa zawadi hiyo kidogo kwa watu wenye uhitaji.

Sauti ya Mwenyekiti wa umoja wa wanawake Wilaya ya Maswa Mkoani hapa Bi,Caroline Shayo