Kahama FM

Msalala yapongezwa kwa ujenzi vyumba vya madarasa

23 August 2026, 3:58 pm

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Wazo Mwang’onda akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya Sekondari ya Segese (Sebastian Mnakaya)

‘‘Mwenge wa uhuru waweka jiwe la msingi katika ujenzi wa vumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Segese’’

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Wazo Mwang’onda ameipongeza Halmashauri ya Msalala Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga kwa ujenzi wa vyumba viwili vya Madarasa katika shule ya Sekondari Segese iliyopo kijiji cha Busungo  kwa gharama ya   zaidi ya shilingi Milioni  45.5.

Mwang’onda ametoa pongezi hizo leo alipokuwa akiweka jiwe la msingi kwenye  vyumba  vya madarasa hayo  ambavyo  vinatarajia kukamilila mwezi Septemba mwaka huu, ambapo amesema Halmashauri hiyo imeanza kazi ya maandalizi kwaajili ya kupokea wanafunzi mwaka 2028 amvapo elimu imekuwa ya lazima kwa mtoto kusoma miaka kumi.

Aidha, Mwang’omba amempongeza mkurugenzi pamoja na tume yake kwa kuendelea kuteleza na kusimamia miradi vizuri, huku akiwataka kuendelea kutekeleza miradi mingine ka huu walioutekeleza.

Sauti ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Wazo Mwang’onda

 Mkuu wa shule ya sekondari segese JohnMarry Prudence, aktoa taarifa kwa kiongozi huyo amesema shule hiyo ina wanafunzi 144 kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne  huku akieleza mradi umetekelezwa kwa force akaunt  na wazabuni  wa vifaa  walipatikana kupitia mfumo  wa manunuzi ya Umma (NeST).

Sauti ya Mkuu wa shule ya sekondari segese JohnMarry Prudence

Mbunge wa jimbo la Msalala Mabula Magangila amesema kuna shule za msingi 125 na sekondari 29 na mpango mkakati kila kijiji kuwe na shule ili watoto wasitembee umbali mrefu kutafuta elimu.

Sauti ya Mbunge wa jimbo la Msalala Mabula Magangila