Kahama FM
Kahama FM
3 June 2026, 5:20 pm

”Wananchi katika Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga wako tayari kwa mabadiliko ya mji wa Kahama kuwa wa kisasa ifikapo 2050”
Wananchi wa kata Zongomela, Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga wameishukuru serikali kwa kuwaletea mradi wa mpango kabambe wa kidigitali, utakao kwenda kuboresha maeneo yao ya makazi kwa kupangwa katika mpangilio mzuri na wakisasa.
Wakizungumza leo viongozi mbalimbali wa kata hiyo kwenye mafunzo ya siku moja ya namna ya mradi huo wa Mpango Kabambe wa kidikitali utakavyotekelezwa katika Manispaa ya Kahama chini ya mradi wa uboreshaji wa miji nchini (TACTIC).

Baadhi ya wananchi wa kata ya Zongomela, akiwemo Marietha Richard na Daud Sasa, wamesema kuwa kuwepo kwa mradi huo utasaidia makazi yao kuwa bora na yenye thamani baada ya kutengenezwa kwa miundombinu mbalimbali kupita mradi huo.
Aidha, wananchi hao wameiomba serikali kupitia mradi huo, kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara kwa kujenga mitaro na barabara kupitika, huku wakiwaomba wananchi kutoa ushirikiano pale ambapo pahitajika wananchi kupisha aridhi kwa ajili ya shughuli za kijamii.

Kwa upande wake, msimamizi wa Mradi wa Mpango Kabambe wa Kidigitali kutoka kampuni ya Urban Solution (ICE EXPERT) Elias Nyabusani amesema mradi huo unawashirikisha wananchi moja kwa moja kwa kutoa maoni yao ili yaingizwe kwenye mpango na kuanza kutekelezwa wake.
Hata hivyo, baada ya miaka 25 ijayo Kahama itakuwa ni mjini wa kisasa na wa mfano katika manispaa nyingine zote chini, huku mradi huo ukitekelezwa kwenye kata zote 20 katika manispaa hiyo.