Kahama FM

Manispaa ya Kahama kuondokana na migogoro ya ardhi, baada ya mradi wa Mpango Kabambe kidikitali kuanza

1 June 2026, 5:41 pm

Mtaalamu Mshauri kutoka Kampuni ya Urban Solution (ICE EXPERT) Hamisi Mkoma akizungumza na viongozi mbalimbali wa kata ya Malunga (picha na Sebastian Mnakaya)

”Kuanza kwa mradi wa Mpango Kabambe Kidigitali kukamilika utaweza kutatua migogoro mbalimbali ya ardhi, pamoja na kuendelea kupanga mji”

Imeelezwa kuwa miaka 25 ijayo, Wananchi wa Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga kuondokana na migogoro ya ardhi baada ya kukamilika kwa mradi wa mpango kabambe wa kidigitali (Master Plan) utakapokamilika.

Lengo la mpango huo unalenga kudhibiti ujenzi na makazi holela Pamoja na kupanga mji kuwa wa kisasa na kutenga maeneo mbalimbali kwa shughuli za kijamii, kiuchini na kiibada.

Akizungumza katika mafunzo na viongozi mbalimbali wa kata ya Malunga, mtaalamu Mshauri kutoka Kampuni ya Urban Solution (ICE EXPERT) Hamisi Mkoma, amesema mradi huo utakapokamika mji utabaridi nakuwa wa kisasa Pamoja na kupunguza changamoto katika sekta miundombinu ya barabara na makazi, huku ardhi  ikipanda thamani.

Sauti ya mtaalamu Mshauri kutoka Kampuni ya Urban Solution (ICE EXPERT) Hamisi Mkoma
Diwani wa kata ya Malunga Hamed Haruna

Kwa upande wake diwani wa kata ya Malunga Hamed Haruna, amesema kuwa mradi huo utaweza kuwasaidia wananchi kupanda kwa thamani ya ardhi na kuwaomba wananchi waupokee mpango kabambe wa kiditali.

Sauti ya diwani wa kata ya Malunga Hamed Haruna

Baadhi wa wananchi wa kata ya Malunga wakizungumza kwa nyakati tofauti akiwemo Michael Msano na Marco Makune, wamesema kuwa mpango huo utakapo kamilika utasaidia kuondoa migogoro ya ardhi, pamoja na mji kupangika na kuwa salama

Sauti za wananchi wa Malunga Michael Msano na Marco Makune

Mradi huo unakwenda kutekelezwa katika kata 20 za Manispaa ya Kinaga, Isagehe, Mondo, Ngongwa, Nyandekwa, Kilago na Wendele zinakwenda kubadilika kutoka vijiji na vitongoji na kuwa mitaa.