Kahama FM
Kahama FM
25 June 2026, 6:25 pm

”Tunapaswa kuisaidia jamii hii ambayo inaishi katika mazingira maguru kwa chochote ulichojaaliwa na Mwenyezi Mungu”
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kahama imetoa msaada wa mahitaji mbalimbali katika Kituo cha Kulelea Watoto wanaotokana na Mazingira Magumu cha Mvuma, kilichopo Kata ya Nyasubi, kuelekea maadhimisho ya miaka 30 ya kuanzishwa kwa TRA tangu mwaka 1995.

Akikabidhi msaada huo, Meneja wa TRA Mkoa wa kikodi Kahama, Wisaka Kamwamu, amesema mamlaka hiyo imeamua kurejesha shukrani kwa jamii kwa kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum na kusisitiza umuhimu wa wananchi kulipa kodi kwa hiari kwa kuwa ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa.
Kwa upande wake Mkaguzi wa Kodi, Estar Malya, amesisitiza umuhimu wa TRA kushirikiana na jamii, huku akieleza kuwa matumizi ya teknolojia yamerahisisha upatikanaji wa huduma mbalimbali za kodi kwa wananchi bila usumbufu.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Kituo cha Mvuma, Everist Magambo, ameishukuru TRA kwa msaada huo na kueleza kuwa kituo hicho kinakabiliwa na changamoto za ukosefu wa bima ya afya kwa watoto, nishati mbadala na vifaa vya michezo.
Mahitaji yaliyotolewa ni pamoja na mchele, unga, mafuta ya kupikia, sukari na madaftar, ambapo kwa sasa Kituo hicho kwa sasa kinahudumia watoto 50, wakiwemo mabinti 30 na wavulana 20.