Kahama FM

Kahama ya kidijitali yanukia

13 July 2026, 5:40 pm

Afisa Mipango Miji Mkuu, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayesimamia mradi ya TACTIC, Alex Mwamaso (Sebastian Mnakaya)

‘‘Kukamilika kwa Mpango Kabambe wa Kidijitali itasaidia kuondoa makazi holela katka Manispaa ya Kahama’’

Halmashauri ya Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga imetakiwa kuendelea kutoa ushirikiano katika kutekeleza mradi wa Mpango Kabambe wa Kidigitali na msimamizi wa mradi, unaotarajiwa kutekelezwa katika kata 20 za manispaa hiyo.

Kauli hiyo limetolewa na Afisa Mipango Miji Mkuu, kutoka ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayesimamia mradi ya TACTIC, Alex Mwamaso katika kikao cha kamati ya mradi wa Mpango Kabambe wa Kidijitali Manispaa ya Kahama.

Mwamaso, amewataka viongozi mbalimbali wa Manispaa hiyo na msimamizi wa mradi huo kushirikiana kikamilifu ili kumaliza kwa wakati utekelezaji wa mradi huo pamoja na kuendelea kuwaelimisha wananchi kuuelewa mpango huo.

Aidha, Mwamaso amesema kuwa kati ya miji 18 nchini, Manispaa ya Kahama pekee imefanikiwa kuwa ya mfano katika utekelezaji wa mradi wa Mpango Kabambe wa kidijitali unaotekelezwa huku miji mingine kuja kujifunza Kahama.

Sauti ya afisa Mipango Miji Mkuu, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayesimamia mradi ya TACTIC, Alex Mwamaso

Kwa upande wake, meneja mradi wa Mpango Kabambe wa Kidijitali kutoke Urban Solution ltd William Kitonka, amesema kuwa wako tayari kushirikiana katika kutekeleza mradi huo, huku akiwaomba watumishi kuendelea kujifunza ili watakapo wakabidhi mradi huo watekeleze kusahihi kama ilivyokusudiwa.

Sauti meneja mradi wa Mpango Kabambe wa Kidijitali kutoke Urban Solution Ltd William Kitonka

Kaimu mkurugenzi mtendaji wa Halamshauri ya Mnaspaa ya Kahama, steven Magala amesema kuwa waendelea kutoa ushirikiano kwa msimazi wa mradi Urban Solution Ltd, huku akiwataka wanapokutana na changamoto wasisite kuziwakilisha kwako.

Sauti ya Kaimu mkurugenzi mtendaji wa Halamshauri ya Mnaspaa ya Kahama, steven Magala