Kahama FM

Waraibu waomba serikali izidi kukabiliana na wauzaji wa dawa za kulevya

22 August 2026, 8:12 pm

Mwenge wa uhuru ukizindua jengo la kliniki ya tiba saidizi kwa waraibu katika hospitali ya Mananispaa ya Kahama (Sebastian Mnakaya)

Waraibu wa matumizi ya dawa za kulevya wanaopatiwa matibabu katika Jengo la Waraibu lililopo Hospitali ya Manispaa ya Kahama mkaoni Shinyanga, wameiomba Serikali kuongeza juhudi za kupambana na wauzaji na wasambazaji wa dawa hizo.

Ombi hilo wamelitoa wakati Mwenge wa Uhuru ukizidua jengo hilo jipya lililojengwa kwa ajiri  ya malezi ya waraibu, lenye thamani ya zaidi ya  shilingi Milion 400 lililoanza kutoa huduma mwezi wa Mei mwaka huu, na Linalenga kuwapatia matibabu, malezi na ushauri waraibu ili waweze kurejea katika Hali yao kawaida.

Baadhi ya warahibu wanaotoka maeneo mbalimbali wilayani humo, akiwemo Mutazi Maganga na Asia Wanga ameomba serikali kutilia mkazo la kuendelea kudhibiti madaya ya kulevya ili vijana waendeleo kuwa salama kwa kutopatikana kwa madawa hayo.

Sauti ya waraibu wa matumizi ya dawa za kulevya Mutazi Maganga na Asia Wanga

Akizungumza baada ya uzinduzi na kupokea maombi ya waraibu, Mkimbiza Mwenge Kitaifa, Wazo Mang’onda, amesema kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA)na Jeshi la Polisi watahakikisha wanaongeza juhudi za kukabiliana na changamoto hiyo.

Sauti ya Kiongozi wa Mkimbiza Mwenge Kitaifa Wazo Mang’onda

Kwa upande wake Dkt, Grace Nzangamba, Msimamizi wa Waraibu Manispaa ya Kahama amesema mpaka sasa kituo kina waraibu 35 wanaopatiwa matibabu, huku kiisisitiza jamii kutosita kuwapeleka kituoni watu wenye changamoto hizo ili wapatiwe matibabu mapema kabla hali haijazidi kuwa mbaya.

Sauti ya Dkt, Grace Nzangamba, Msimamizi wa Waraibu Manispaa ya Kahama

Hata hivyo, Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 Unaujumbe Usemao “Tanzania yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo”.