Kahama FM
Kahama FM
23 August 2026, 5:14 pm

“Serikali kuu ilileta shilingi Milioni 250 na Halmashauri ya Msasa imetoa zaidi ya shilingi Milioni 19 kwa kuboresha miundombinu ya kituo hicho’’
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Wazo Mwang’onda ameweka jiwe la msingi kwenye jengo la wodi ya wazazi kwenye kituo cha Afya Kakola kata ya Bulyanhulu Halmashauri ya Msalala Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga kilichogharimu zaidi ya shilingi Milioni 269.

Kabla ya kuweka jiwe hilo Mganga mfawidhi wa kituo hicho dkt Emanuel Boniface akisoma taarifa ya ujenzi huo leo amesema ujenzi ulianza rasmi mwezi Oktoba mwaka 2025 na kukamilika mwaka 2026 mwezi Julai.

Mbunge wa jimbo la Msalala Mabula Magangila amesema kuwa kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kata ya kakola ina takribani wakazi 51,000 lakini walikuwa hawana kituo cha afya kulikuwa na Zahanati tu.

Mwang’onda amesema kuwa katika kata hiyo kulikuwa hakuna kituo afya hali iliyosababisha wananchi kwenda kutafuta huduma mbali, ila kwa sasa watapata huduma ya afya karibu, huku akipongeza halmashauri hiyo kusimamia vizuri wakandarasi kwani jengo hilo limejengwa kwa kiwango kizuri.
