Kahama FM
Kahama FM
2 September 2026, 2:38 pm

Madiwani wa Halmashauri ya Ushetu mkoani Shinyanga wametakiwa kwenda kuwajengea uelewa wananchi wa Kata zao kuhusu uchukuaji wa tahadhari baada ya Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini -TMA kutangaza ujio wa mvua za juu ya wastani El Nino.
Tahadhari hiyo imetolewa hivi karibu na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) ya kuwataka wananchi kuchuka tahadhari juu ya mvua hizo, ikiwa pamoja na kutunza vyakula walivyovuna msimu huu.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Gagi Lala Gagi wakati wa kikao cha Maalum wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo kwa ajili ya ufungaji wa Hesabu za Halmashauri, Afisa Kilimo wa Halmashauri hiyo Mapenzi Mshana akiwakumbusha wakulima kuendelea kujiandaa na msimu mpya wa kilimo kwa kufanya maandalizi ya mbegu za mazao zinazokubalika na hali hiyo.

Kwa upande wao, baadhi ya diwani wa halmashauri hiyo akiwemo diwani wa Kata ya Kinamapula Samwel Sharif na diwani wa kata ya Igunda Tabu Katoto wameahidi kupeleka elimu hiyo kwa wananchi wao kwa njia ya kufanya mikutano ili kujiandaa na mvua za El Nino.
