Sibuka FM

RC Simiyu aagiza kusimamishwa kazi Daktari aliyesababisha kifo cha Mama aliyeenda kujifungua.

24 June 2021, 10:05 am

Mkuu  wa mkoa  wa  Simiyu   Mh  David   Kafulila  amemuagiza  Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Halmashauri   ya  wilaya  ya  Maswa   kumsimamisha  kazi   mganga  Mfawidhi  wa   Zahati  ya  Senani   iliyopo  kata  ya  Senani  wilayani  hapa   Ally  Soud   kwa  kusababisha   Kifo  cha  Mama  na  Mtoto  aliyeenda  kujifungua  katika  Zahanati  hiyo..

Mh,  Kafulila  ametoa  agizo  hilo   wakati  wa   Mkutano  wa  Baraza  la  Madiwani la  kujadili  Mapendekezo  ya  Mdhibiti  na  Mkaguzi  Mkuu  wa  Hesabu  za  Serikali  (CAG)  kwa  mwaka 2019/2020.

Sauti ya RC Simiyu David Kafulila

       

Akielezea  tukio  hilo  Mganga  mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa  Dokta   Mpolo  Adorati  amesema  kuwa  mama huyo  anayejulikana  kwa   jina  la  Christina  Jilala  alifika  kwenye   Zahanati  ya   Senani  kwa  ajili  ya   kujifungua  tarehe  20. 06  mwaka  huu  lakini  hakupata  Huduma  baada  ya  Dakitari  huyo  kwenda  kuamushwa  na  Mhudumu  wa  Afya  ngazi  ya  Jamii  na  kumkatalia.

Sauti ya DMO Maswa Dr Mpolo

      

Dokta  Mpolo  amesema  kuwa  Kifo   hicho  kilikuwa  kinaepukika  endapo  mtaalamu  huyo  angekuwepo  katika  kituo  Chake  cha   kazi  angeona  shida  hiyo  mapema  na  kutoa   taarifa  ngazi  ya  wilaya   licha  ya  mama  huyo  kuwa  na  Uzazi  Pingamizi.

Sauti ya DMO Maswa Dr Mpolo

    

Katika  hatua  nyingine  mkuu  wa  mkoa  Mh  Davidi  Kafulila  amesema  kuwa  mkoa  umejipanga  kuongeza  tija  ya  uzalishaji  wa  Zao  la  Pamba   kutoka  kilo  mia mbili  kwa  Ekari  moja   kwa  sasa  hadi  kufikia   kilo  Mia  Nane  kwa  Ekari  moja.

Sauti ya RC Simiyu David Kafulila

Picha mbalimbali.