Sibuka FM

Mradi wa Chujui la Maji Maswa wanufaisha wakazi zaidi ya Laki moja.

23 June 2021, 10:15 am

Zaidi  ya   wakazi  Laki  moja  wa  Mji  wa  Maswa  na  vijiji  jirani  wamenufaika   na  Mradi  wa    Mtambo  wa  kutibu  na  Kusafisha   Maji.

Hayo  yamesemwa  na  Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Mamlaka  ya  Maji  na  Usafi  wa  Mazingira  Maswa-MAUWASA   Mhandisi    Nandi  Mathias  wakati  wa  kutembelea  Ujenzi   wa Mradi  huo  uliogharimu  Zaidi  ya  Bilioni  tatu.

Sauti ya Mhandisi wa maji Maswa Nandi Mathias

           

Mhandisi  Nandi  amesema  kuwa    kukamilika  kwa  mradi  huo   maji  umeondoa  adha  ya upatikanaji  wa  maji  kwani  kwa  sasa  Unazalisha  lita  za  Ujazo  Elfu  kumi  ikiwa  Mahitaji   maji  kwa  Mji  wa  Maswa  ni  lita  za  Ujazo  elfu  Saba.

Sauti ya Mhandisi wa maji Maswa Nandi Mathias

          

Bahati  Mwaipopo  ni  Mhandisi  kutoka  kampuni   ya  PET  CO-OPARATION  LIMITED   ambao  ndio  wajenzi   wa  Mradi  huo   amesema  kuwa  kwa  sasa   Mradi  huo  umekamilika  kwa   asilimia  mia  moja.

Sauti ya Mhandisi wa Ujenzi wa Mradi Bahati Mwaipopo

          

Aida   baadhi  ya  wananchi na  wadau  wa  maji  mjini  maswa  wameishukuru  serikali  kwa  kujenga  chujio  hilo  kwani  kwa  sasa  maji  yanatoka  meupe   na  ang’avu  tofauti  na hapo awali  kabla  ya  kukamili kwa  mradi  wa  ujenzi  wa   Chujio  hilo..

Baadhi ya wadau na watumiaji wa Maji Maswa

       

Picha za muonekano wa Mradi wa Chujio na Chanzo chake- Bwawa la New Sola.