Sibuka FM

Dc  Maswa  Aswege   Kaminyoge  atoa  Maagizo  Mazito  kuhusu  chanjo  ya  Mifugo.

20 April 2023, 9:34 am

Mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa  Mkoani  Simiyu  Mhe Aswege  Kaminyoge  ametoa  Maagizo  kwa  Wafugaji  Wote  kupeleka   Mifugo  yao  kwenda  kuchanja  Sehemu  ambazo  zimeandaliwa  na  kijiji  husika  ili  kujikinga  na  Magonjwa  hatari  ya  Mifugo.

            Sauti ya DC  Maswa Aswege kaminyoge kuhusu  Maagizo  ya  chanjo ya Mifugo

Mhe,  Kaminyoge  amesema  kuwa   zoezi  hili  la  Chanjo  lisihusishwe  na   Zoezi  la  uwekaji  wa  Heleni  za  Utambuzi  wa  Mifugo   hivyo  kutoa  Maelekezo  kwa  Afisa  Mifugo  Wilaya  ya  Maswa  kuhakikisha  Mifugo  wote Wanatambuliwa  na   Kupatiwa  Chanjo  hiyo.

        Sauti ya DC  Maswa Aswege kaminyoge kuhusisha zoezi la Hereni na chanjo

Awali  katika  Kikao  hicho  kilichohusisha  Viongozi  wa  Vijiji  na  Kata  katika  kata  ya  Mwamashimba, Mkuu  wa  Wilaya  alihoji  kuhusu  kusua sua  kwa  zoezi  hilo, Baadhi  ya  Viongozi  hao  akaeleza  changamoto  zilizojitokeza  kuhusu  zoezi  la  Chanjo  ya Magonjwa  ya  Mifugo  Kuhusishwa  na  Zoezi la  Utambuzi  wa  Heleni  za  Mifugo ambalo  lilileta  Sitofahamu  kwa  baadhi  ya  Maeneo.

    Badhi ya Sauti za Viongozi  wa  vijiji vya Mwamashimba