Sengerema FM

Baptist Sengerema waliombea taifa kuelekea uchaguzi mkuu 2025

10 June 2025, 6:14 pm

Mwakilishi wa aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Sengerema na Waziri wa Nishati na madini mstaafu Wiliamu Mganga Ngeleja akikabidhi fedha kwa ajili ya ujenzi na ununuzi wa vyombo vya muziki kanisa la Baptist

Kufuatia uwepo wa matukio ya uvunjifu wa amani kuelekea uchaguzi mkuu 2025 viongozi na wamini wa kanisa la Baptist Sengerema wameungana na kufanya maombi ya kuliombea taifa ili liendelee kuwa kisiwa cha amani kama inavyotambulika kuwa Tanzania ni kisiwa cha Amani.

Na,Joyce Rollingstone

Umoja wa Makanisa ya Baptist Wilayani Sengerema wamefanya maombi maalum kwa ajili ya kuombea Amani Taifa la Tanzania, katika kuelekea uchaguzi Mkuu Octobar Mwaka huu.

Maombi hayo yamefanyika katika kanisa la Baptist ishingisha lililopo katika kata ya Sima Wilayani Sengerema,ambapo mshauli wa makanisa ya Baptist askofu mstaafu wa kanda ya ziwa Boniphas.K. Mponeja wa kanisa la Baptist Gethsemane Igogo A,amewaomba  waumini wote kuilinda Amani iliyopo.

Sauti ya askofu mstaafu wa kanda ya ziwa Mch. Boniphas.K. Mponeja akizungumzia amani nchini

Aidha waumini walioshiriki maombi hayo,wameahidi kuwa watailinda na kuidumisha Amani iliyopo kwani ikipotea ni vigumu kuilejesha.

Sauti za baadhi ya waumini wa kanisa la Baptist Sengerema wakizungumzia namna ya kuilinda amani iliyopo nchini

Sambamba na hayo,pia umoja huo umejumuisha upokeaji wa fedha za ujenzi wa kanisa la Baptist Igogo A,ununuzi wa kiwanja cha kanisa,pamoja na ununuzi wa vyombo vya kwaya,ambapo mwakilishi wa aliyekuwa mbunge wa jimbo la Sengerema Mh Wiliamu Mganga Ngeleja, Ndug,Lugega Festo Petro,amekabidhi fedha hizo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyokuwa imetolewa huku akiwataka kuendelea kuilinda Amani iliyopo.

Sauti ya Mwakilishi wa Wiliam Ngereja Ndug,Lugega Festo Petro akiwasilisha fedha kwa ajili la ujenzi wa kanisa

Naye asikofu wa makanisa ya  Baptist sengerema Eliasi Kusaya, ameshukuru aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Sengerema Dkt.Willium Mganga Ngereja kwa kuunga mkono juhudi za neon la Mungu.

Sauti ya asikofu wa makanisa ya  Baptist sengerema Eliasi Kusaya akimshukuru aliyekuwa mbunge wa Sengerema

Hata hivyo, maombi hayo yamehudhuliwa na viongozi mbalimbali wa makanisa ya Baptis, pamaja na waumini .