Sengerema FM

RUWASA watoa msaada kwa wafungwa magereza ya Kasungamile

21 March 2025, 7:31 pm

Viongozi wa Magereza ya Kasungamile Sengerema wakipokea misaada kwa wafungwa iliyotolewa na RUWASA Sengerema. Picha na Emmanuel Twimanye

Kila mwaka Machi 22 huwa ni Siku ya Maji ambayo huadhimishwa kimataifa kutokana na  na Azimio Na. 47/193 la Umoja wa Mataifa (UN), ambapo Wakala wa Maji Vijijini RUWASA wialayani Sengerema umetoa msaada kwa wafungwa na kupanda miti kwenye vyanzo vya maji.

Na,Emmanuel Twimanye

Wakala wa Maji vijijini (RUWASA) wilayani Sengerema mkoani Mwanza wametoa msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo  taulo za kike kwa wafungwa na mahabusu katika gereza la Kasungamile .

Akikabidhi msaada huo kwa viongozi wa Gereza hilo kaimu Meneja wa wakala wa maji vijiiini Wilayani Sengerema Tyson Magagala   amesema kuwa wametoa msaada huo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha wiki ya maji Duniani.

Sauti ya kaimu Meneja wa wakala wa maji vijiiini Wilayani Sengerema Tyson Magagala akizungumzia msaada walio pelleka kwa wafungwa

Kaimu mkuu wa Gereza la Kasungamile amewashukuru wakala wa maji kwa kutoa  msaada huo kwani utawasaidia wafungwa na mahabusu .

Sauti ya kaimu mkuu wa magereza Kasungamile Rafael Mtasagala akizungumzia msaada uliotolewa na RUWASA

Katika hatua nyingine wakala wa maji wametumia sehemu ya maadhimisho hayo ya wiki ya maji kwa kupanda miti mia tano katika chanzo cha maji  Katwe  Halmshauri ya Buchosa ili kuitunza mazingira.

Sauti ya kaimu Meneja wa wakala wa maji vijiiini Wilayani Sengerema Tyson Magagala akizungumzia zoezi la upandaji miti Buchosa

Nao baadhi ya wananachi wa Katwe wamepongeza Ruwasa kwa kupanda miti hiyo huku wakiahidi kuitunza .

Sauti za wananchi wakiipongeza RUWASA Sengerema