Sengerema FM

Waipongeza Sengerema FM kwa kutoa elimu ya ugonjwa marburg

15 March 2025, 1:29 pm

Picha ya jengo la Radio Sengerema lililopo mjini Sengerema mkoani Mwanza

Serikali ya Tanzania kupitia Waziri wa Afya nchini Mh. Jenista Mhagama imetangaza kufanikiwa kuudhibiti ugonjwa wa marburg, ambao ulitangazwa kuibuka nchini mwezi Januari 2025 katika halmashauri ya wilaya ya Bihalamulo mkoani Kagera.

Na,Elisha Magege

Kufuatia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Afya kutangaza kufanikiwa kuuondoa ugonjwa wa homa ya marburg nchini, wananchi wilayani Sengerema wameipongeza Radio Sengerema kwa kushirikiana na serikali  kutoa elimu juu ya ugonjwa huo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti kutoka maeneo mbalimbali wananchi hao wamesema kupitia radio Sengerema wamepata elimu ya kujikinga na marburg jambo lililopelekea ugonjwa huo kuishia mkoani Kagera pekee.

Sauti ya baadhi ya wananchi Sengerema wakitoa pongezi zao kwa Serkali n a Radio Sengerema kwa kutoa elimu ya ugonjwa wa marburg

Kufuatia pongezi hizo mratibu wa kituo cha habari na mawasiliano Sengerema Telecentre Bwn. Peter Marlessa amewashukuru wananchi wilayani hapo kwa kuendelea kuiamini radio yao huku akiahidi kuwa wataendelea kutoa elimu juu masuala mbalimbali yanayoihusu jamii.

Sauti ya mratibu wa kituo cha habari na mawasiliano Sengerema Telecentre Bwn, Piter Marlesa akizungumzia ushirikiano wa radio na wadau

Mbali na pongezi hizo wananchi pia wameiomba serikali kuendelea kutoa elimu za magonjwa mbalimbali ya mlipuko, ikiwemo ugonjwa wa M-POX ulioripotiwa kutokea nchini. 

Hata hivyo taarifa iliyotolewa na Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama tar 13 Machi 2025  imesema Tanzania imefanikiwa kuudhibiti ugonjwa wa mlipuko wa marburg kutokana na kutokuwepo kwa mgonjwa mwingine yeyote tangu mgonjwa wa mwisho alipopatikana tarehe 28 Januari, 2025 na hadi kufikia tarehe 11 Machi, 2025 siku 42 zimepita.

Waziri wa Afya Jenista Mhagamo akizungumza na wandishi wa habari Bihalamulo mkoani Kagera.Picha na wizara ya afya