Sengerema FM

Diwani apongeza maboresho miundombinu ya elimu Mayuya

24 September 2024, 8:33 pm

Diwani kata ya Tabaruka Mh. Sospiter Simon Busumabhu akikabizi viti na meza kwa ajili ya walimu shule ya msingi Mayuya.Picha na Emmanuel Twimanye

Shule ya msingi Mayuya ni miongoni mwa shule zilizokuwa zikifanya vibaya kwenye mitihani yake kutokana na uhaba wa vitendea kazi kwa walimu pamoja na miundombinu iliyokuwepo kuchakaa, jambo lililomlazimu diwani wa kata hiyo kuchukua hatua ya kuanza kuboresha miundombinu ya walimu kwa lengo la kuinua ufaulu wa wanafunzi shuleni hapo.

Na;Emmanuel Twimanye

Diwani wa kata ya Tabaruka Mh. Sospeter Busumnabu ameupongeza uongozi wa shule ya msingi Mayuya kwa kukarabati miundombinu ya shule  pamoja na kutengeneza  samani za  ofisi za walimu zenye   zaidi ya shilingi milioni moja  kwa kutumia fedha za ukarabati  na rasilimali za shule.

Pongezi hizo zimetolewa na Diwani huyo wakati akikabidhi samani hizo kwa  uongozi wa shule hiyo kwa kuwa wa kwanza kukarabati miundombinu kati ya shule zote zilizopo katika  kata ya Tabaruka  ikiwa ni utekelezaji  wa maelekezo yaliyotolewa katika  kikao cha maendeleo ya kata  hiyo kwa shule zote  kuhakikisha zinafanya hivyo.

Sauti ya Diwani wa kata ya Tabaruka akiupongeza uongozi wa Shule ya Msingi Mayuya kwa ukarabati samani mbalimbali kwa fedha na raslimali za shule.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mayuya Bwn ,Ladislaus Zacharia pamoja na kupongeza hatua hiyo amewaomba walimu kuendelea kuwafudisha wanafunzi kwa bidii ili kuwasaidia wanafunzi kufikia ndoto zao na kupata viongozi watakaolisaidia Taifa  hapo badae  kutoka katika shule hiyo.

Sauti ya Mwenyekiti wa Kijiji cha Mayuya Bw. Ladislaus Zacharia akizungumzia shule hiyo

Mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi Mayuya    Nkandala Kahemejo  ameupongeza  uongozi wa shule kwa kupiga hatua   kubwa  kwa kuboresha miundombunu .

Sauti ya Mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi Mayuya    Nkandala Kahemejo akizungumzia jitihadi walizochukua kuboresha miundombinu shuleni hapo.

Uongozi wa shule hiyo umeahidi kufanya mabadiliko makubwa Zaidi ikiwa ni pamoja na kuongeza ufaulu  kwa wanafunzi .

Uongozi wa shule ukiahidi kuendelea kuboresha miundombinu ya shule hiyo

Nao baadhi ya walimu wameshukuru  Diwani wa kata hiyo na Uongozi wa shule  kwa kukarabati miundombiny hiyo  kwa kuwa itawasaidia  kufundisha katika mazingira rafiki .

Sauti za baadhi ya walimu shule ya msingi Mayuya
Baadhi ya viti na meza alizokabidhi Mh. Diwani kwa uongozi wa shule ya msingi Mayuya.
Baadhi ya viti na meza alizokabidhi Mh. Diwani kwa uongozi wa shule ya msingi Mayuya.