Karagwe FM
Karagwe FM
28 August 2026, 12:33

Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kukimbizwa kilomite 50.5 wilayani Karagwe siku ya Ijumaa Septemba 4. 2026 ambapo pamoja na miradi mingine utazindua ghala la kahawa la kiwanda cha chama kikuu cha ushirika KDCU Ltd wilayani Karagwe mkoani Kagea
Na Shabani Ngarama, Karagwe
Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kupokelewa Septemba 4. 2026 wilayani Karagwe ukitokea wilaya ya Kyerwa na kukimbizwa ukipita katika miradi sita ya maendeleo iliyotekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 2.9 ikiwa ni pamoja na mradi wa ghala la kiwanda cha kahawa la chama kikuu cha ushirika KDCU Ltd litakalozinduliwa siku hiyo
Mkuu wa wilaya ya Karagwe mkoani Kagera Julius Laiser amesema kuwa mapokezi ya mwenge yatafanyika katika eneo la Maya kata ya Nyabionza baada ya mkesha wa mapokezi na kwamba utapita katika mradi wa kituo cha afya Nyabionza kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi

Laiser amesema maandalizi ya mapokezi ya mwenge yamekamiliks na kwamba kutakuwa na mikesha miwili kuanzia Septemba 3 na kisha uwanja katika stendi ya mabasi Kayanga Septemba 4. 2026 baada ya mwenge huo kukimbizwa umbali wa Km 50.5 kuanzia eneo la mapokezi