Karagwe FM
Karagwe FM
2 May 2026, 10:05 am

Malalamiko ya wafanyakazi nchini juu ya mazingira duni ya kazi imekuwa kilio chao kila wanapoadhimisha siku ya wafanyakazi duniani hasa wakiiomba serikali kuchukua hatua kwa waajiri
Na Respicius John, Missenyi
Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali Yahya Ramadhan Kido amewaagiza waajiri katika sekta binafsi kulipa kwa wakati mishahara ya watumishi wao kulingana na kima cha chini cha msahara kilichotangazwa na serikali sambamba na kuwasainisha mikataba ya hali bora ya kazi
Kanali Kido ametoa maagizo hayo wakati akihutubia maelfu ya wafanyakazi wa mkoa wa Kagera wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Mei mosi yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya kiwanda cha sukari Kagera
Katika risala ya wafanyakazi iliyosomwa na mratibu wa shirikisho la wafanyakazi TUCTA mkoa wa Kagera Njile Antony imebainisha changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyakazi mkoani Kagera ikiwa ni pamoja na mishahara duni kwa watumishi wa sekta binafsi

