Karagwe FM

CBIDO wajenga uwezo kwa walimu elimu maalum Karagwe

29 August 2026, 22:09

Mratibu wa shughuli za shirika la CBIDO Julieth Aloyce. Picha na Jovinus Ezekiel

Shirika la kuhudumia vijana na watoto wenye ulemavu mkoani Kagera CBIDO limeendelea kupanua mtandao wa ushirikiano na taasisi za serikali katika utoaji elimu ya kuzuia ulemavu

Na Jovinus Ezekiel, Karagwe

Uongozi wa shirika la kuhudumia watoto na vijana wenye ulemavu wilayani Karagwe CBIDO umeahidi kuendeleza mkakati wa kutoa elimu  kwa   walimu wa shule zenye vitengo vya elimu   maalum hali itakayosaidia kutatua baadhi ya changamoto zinazokabili kundi hilo.

Akizungumuza Agosti 28. 2026 mara baada ya kumalizika kikao cha pamoja kilichowajumuisha baadhi ya walimu wakuu na walimu wanaofundisha shule zenye vitengo vya  watoto wenye mahitaji maalum katika ukumbi wa mikutano Benjamini Hall uliopo Nyakanongo kata ya Kayanga wilayani Karagwe, mratibu wa shughuli za shirika la CBIDO Julieth Aloyce amesema kuwa lengo la kikao hicho ambacho kimefanyika katika ukumbi wa Benjamin All mjini kayanga ni kuweka mpango mkakati  wa kuwajengea uwezo walimu wanaofundisha  shule zenye wanafunzi wenye mahitaji maalum ili kubaini baadhi ya changamoto zinazowakabili na jinsi ya kuzitatua.

Sauti ya mratibu wa shughuli za shirika la CBIDO Julieth Aloyce
Afisa elimu maalum idara ya elimu msingi halmashauri ya wilaya ya Karagw Merrynes Alphonce. Jovinus Ezekiel

Naye Merrynes Alphonce afisa elimu maalum  idara ya elimu msingi halmashauri ya wilaya Karagwe anaamini kuwa elimu  ambayo imetolewa italeta tija kubwa kwa walimu hao huku baadhi ya washiriki wa kikao hicho wakishukuru kwa elimu waliyoipata. 

Afisa elimu maalum idara ya elimu msingi halmashauri ya wilaya ya Karagw Merrynes Alphonce pamoja na baadhi ya washiriki wa kikao
Baadhi ya washiriki wa kikao wakifuatilia mawasilisho na elimu mbalimbali. Picha na Jovinus Ezekiel