Sengerema FM

Wazazi watakiwa kuwalinda watoto waliohitimu darasa la 7

9 October 2024, 12:55 pm

Diwani Kata ya Mission Sengerema akizungumza kwenye mahafali Shule ya Msingi matwiga.Picha na Jovna George

Shule ya Msingi Matwiga ni miongoni mwa Shule mpya za msingi zilizojengwa katika kata ya Mission halmashauri ya Sengerema

Na;Jovna George

Diwani wa kata ya misheni Wilayani Sengerema  Francis Mbungai  amewataka wazazi na walezi kuwalinda watoto waliohitimu Darasa la saba  wakati wakisubiri matokeo ya mtihani  ili waweze kutimiza ndoto zao za kielimu.

Hayo yamesemwa na  Diwani huyo katika mahafali ya Darasa la sba katika shule ya Msingi Matwiga  na kusema kuwa  wazazi na walezi watakao washawishi watoto wao   kuolewa ama kufanya kazi za nyumbani    hatua kali za kisheria  zitachukuliwa dhidi yao.   

Sauti ya Diwani wa Kata ya Mission Mh. Mbungai Majumba akizungumza mahafali ya shule ya Msingi Matwiga

Vile vile Wazazi wamewasihi wahitimu wa darasa la saba kuepuka vishawishi mitaani na kuzingatia walichokipata shule ili kufikia malengo yao.

Sauti ya Baadhi ya wazazi wakiwasihi watoto wao kufanya vizuri masomo yao

Awali  Wakisoma lisara mbele ya mgeni rasmi ,Martine Lubango kwa niaba ya wahitimu wa darasa la saba matwiga wamesema kuwa pamoja na shule hiyo kuwa imala na kufanya vizuri katika mitihani mbalimbali bado inakabiliwa na    changamoto  mbalimbali ikiwemo ukosefu wa umeme, barabara, computer, printa na upungufu wa walimu.

Sauti za wanafunzi kupitia risala fupi kwa mgeni Rasimi

 Mgeni rasmi  katika mahafali hayo   Katibu wa kamati ya  elimu na mazingira  wa Jumuiya ya wazazi ya chama cha mapinduzi (CCM ) Wilaya ya Sengerema   Martine Lubango  ameahidi  kutatua baadhi ya chanagamoto zinazoikabili shule hiyo .

Sauti ya mgeni Rasimi Bwn.Martine Lubango

 Mkuu wa shule ya Sekondari Nyampulukano Mwl,Mathias Misungwi Paul ameahidi  kutoa kompyuta kwa  ajili ya kurahisisha katika shughuli za uchapishaji wa mitihani  katika shule ya msingi matwiga.

Sauti ya Mkuu wa shule ya Sekondari Nyampulukano Mwl,Mathias Misungwi Pau

Kwa upande wake    mkuu wa shule ya msingi matwiga  Mwl, ,Boniphase Katalyeba  amewapongeza   viongozi wote walioshiriki na kutoa michango yao katika ujenzi Wa maendeleo ya shule hiyo  pamoja na walimu kwa kuendelea kuendelea kujenga taaluma katika shule hiyo.

Sauti ya mkuu wa shule ya msingi matwiga  Mwl, ,Boniphase Katalyeba