Sengerema FM

Nyang’hwale wanufaika na mbegu toka COPRA

23 January 2026, 7:17 pm

Baadhi ya wakulima wakifurahia kupata Mbegu za alizeti, Picha na Said Mahera

Wakulima katika wilaya ya Nyang’hwale wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dr. Samia Suluhu Hassani kwa kupata mbengu za Alzeti bure sambamba na Mbolea za rudhuku, zenye lengo la kumuinua mkulima nchini.

Na;Said Mahera

Mamlaka ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) imetoa tani 23 za mbengu za alizeti   katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita  kwa ajili ya msimu mpya wa kilimo cha zao hilo.

Afisa Kilimo wa Wilaya ya Nyang’hwale, Ndg. Gudala Kija,  akitoa     tani 1.25 za mbegu za alizeti kwa wananchi wa Kata ya Izunya, kuelekea msimu mpya wa kilimo cha zao hilo la alizeti amesema mbegu hizo wakulima wa kata zote 15 katika halmashaurti hiyo.

Sauti ya Afisa Kilimo wa Wilaya ya Nyang’hwale, Ndg. Gudala Kija,

Kwa upande wake  Afisa Ugani wa Kata ya Izunya, Ndg. Samson Makubate, amesema kabla ya kuanza zoezi la ugawaji wa mbegu hizo, wananchi wamepatiwa elimu ya kutosha kuhusu kilimo bora cha alizeti, ikiwemo namna sahihi ya kupanda, kudhibiti wadudu waharibifu pamoja na matumizi sahihi ya mbolea.

Sauti ya Afisa Ugani wa Kata ya Izunya, Ndg. Samson Makubate
Pichani ni Afisa Ugani wa Kata ya Izunya, Ndg. Samson Makubate.Picha na Said Mahera

Nao wananchi Wananchi wa Kata ya Izunya  wameishukuru Serikali kwa kuwapatia mbegu za alizeti kuelekea msimu mpya wa kilimo cha zao hilo.

Sauti za wananchi Wananchi wa Kata ya Izunya 

Hata hivyo afisa kilimo    amewahimiza wakulima kutumia mbegu hizo kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuhakikisha wanapata mavuno bora na kufanikisha juhudi za serikali za kukuza sekta ya kilimo.