Sengerema FM

Maambukizi ya VVU yazidi kupungua Sengerema

2 December 2025, 3:15 pm

mratibu wa afua za ukimwi na magonjwa ya Gono na homa ya ini halmashauri ya Sengerema Dr.Magreth Buzoya Akizungumza.Picha na Elisha Magege

Utoaji elimu kwa jamii juu ya maambukizi ya VVU na UKIMWI Halmashauri ya Sengerema imesaidia kupunguza kuenea kwa kasi maambukizi mapya VVU.

Na;Elisha Magege

Maabukizi ya Virusi vya ukimwi katika Halmashauri ya Sengerema Mkoani Mwanza yamepungua kutoka asilimia 2.0 mwaka 2023/24 hadi asilimia 1.8 mwaka 2025.

Akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya Ukimwa Duniani yaliyofanyika katika Kijiji cha Chifunfu, mratibu wa afua za ukimwi na magonjwa ya Gono na homa ya ini halmashauri ya Sengerema Dr.Magreth Buzoya, amesema kufuatia elimu wanayoendelea kuitoa kwa umma mambukizi yanazidi kupungua mwaka hadi mwaka.

Sauti ya mratibu wa afua za ukimwi na magonjwa ya Gono na homa ya ini halmashauri ya Sengerema Dr.Magreth Buzoya

Kwa upande wake Ndg. Mohamed Kombo, Mratibu wa kudhibiti ukimwi na afua za ukimwi ngazi ya jamii Halmashauri ya Sengerema, akizungumza kwa niaba ya mgeni Rasimi, amewataka wadau mbalimbali kuungana kwa pamoja kutoa elimu ili kudhibiti mambukizi mapya ya (VVU) katika jamii.

Sauti ya Ndg. Mohamed Kombo, Mratibu wa kudhibiti ukimwi na afua za ukimwi ngazi ya jamii Halmashauri ya Sengerema
Ndg. Mohamed Kombo, Mratibu wa kudhibiti ukimwi na afua za ukimwi ngazi ya jamii Halmashauri ya Sengerema. Picha na Elisha Magege

Aidha baadhi ya wananchi wa kijiji cha chifunfu wameishukuru Serkali ya Halmashauri ya Sengerema kwa kufanya maadhimisho hayo kwenye eneo la kijiweni, kwani wameweza kupima afya zao bure bila malipo.

Sauti za Baadhi ya wananchi walijitokeza kupima afya zao

Maadhimisho ya siku ya Ukimwi Dunia hufanyika kila mwaka Desember mosi ambapo kwa mwaka huu yalikuwa na kauli mbiu ya “Shinda vikwazo imarisha mwitikio, Tokomeza ukimwi,jitambue,Pima afya yako leo”

Baadhi ya wananchi walijitokeza kwenye maadhimisho siku ya Ukimwi Duniani.Picha na Elisha Magege