Sengerema FM

Wasiojulikana waua mmoja kwa kumkata mapanga Sengerema

27 November 2025, 3:02 pm

Baadhi ya waombolezaji wakati wa mazishi ya Ndg.Kajanja Mtebi aliyeuawa kwa kukatwa mapanga.Picha na Emmanuel Twimanye

Matukio ya watu kuuawa kwa kukatwa mapanga wilayani Sengerema yalidhibitiwa kwa muda mrefu, jambo lililowafanya wananchi kushituka baada ya tukio la hivi karibuni kutokea katika kata ya Sima

Na,Emmanuel Twimanye

Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la  Kajanja Mtebi (50) mkazi wa Kijiji cha Sogoso kata ya Sima Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza ameuawa kwa kudaiwa kukatwa katwa kwa mapanga na watu wasiojulikana ,huku chanzo cha tukio hilo bado hakijafahamika .

Wakizungumzia tukio hilo baadhi ya ndugu na majirani wa familia hiyo wamesikitishwa na tukio hilo na kuiomba serikali kufanya uchguzi ili kubaini watu wanaodaiwa kutekeleza unyama huo na kuwachukulia hatua kali za kisheria .

Sauti za baadhi ya ndugu wa familia

 Mwenyekiti wa Kijiji cha Sogoso Martine  Luchagula   amekiri kutokea kwa tukio hilo na kutaja jina la mtu aliyefariki kuwa ni  Kajanja Mtebi .

Sauti ya mnwenyekiti wa Kijiji cha Sogoso Martine  Luchagula 

Kwa upande wake  mkuu wa Wilaya ya Sengerema  Mh,Senyi Ngaga   amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini watu waliohusika na mauaji hayo na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.  

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Sengerema  Mh,Senyi Ngaga
Mkuu wa Wilaya ya Sengerema  Mh,Senyi Ngaga akizungumza na wandishi kuhusu tukio la mtu kukatwa mapanga.Picha na Emmanuel Twimanye