Sengerema FM

Wananchi Sengerema wailalamikia SEUWASA kukatika maji mara kwa mara

16 August 2025, 7:54 pm

Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya maji Sengerema ,Mhandisi Sadala Khamis Sadick. Picha na Peter Marlesa

Licha ya kuwa na mradi mkubwa wa maji wenye thamani zaidi ya Tsh.Bil 22 Wilaya ya Sengerema imekuwa na changamoto ya kukosa maji mara kwa mara hasa kwenye maeneo ya miinuko bila kutolewa ufafanuzi kwa wananchi.

Na,Peter Marlesa

Wananchi Wilayani Sengerema mkoani Mwanza Wameitaka mamlaka ya maji na usafi wa mazingira (Seuwasa)kufanya maboresho ili maeneo ya miinuko yafikiwe na huduma ya maji muda wote.

Hayo yanajili baada ya wananchi kuilalamikia mamlaka hiyo kuwa maeneo hasa yenye miinuko hukaa muda mrefu bila huduma ya maji,na kwamba mgao usio na ratiba maalumu unapunguza ufanisi wa huduma hiyo muhimu katika jamii.

Sauti za wananchi wakilalamikia kukosekana kwa huduma ya maji mara kwa mara Sengerema

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya maji Sengerema ,Mhandisi Sadala Khamis Sadick amesema kuwa changamoto za kijiografia ndio chanzo cha upungufu wa maji kwa baadhi ya maeneo mjini Sengerema, pamoja na hayo amewataka wananchi kulipia huduma hiyo kadri ya matumizi yao kwa wakati.

Sauti za mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya maji Sengerema ,Mhandisi Sadala Khamis Sadick

Mbali na changamoto hizo,Seuwasa imepiga hatua kubwa ya kutandaza mfumo wa maji,ambapo kwa mjini ni zaidi ya asilimia ya tisini na vijijini zadi ya asilimia 70 kwa wilaya yote.