Sengerema FM

Nukta Afrika yaja na mwarobaini kubaini taarifa za uongo

28 July 2025, 5:17 pm

Picha ya pamoja baadhi ya washiriki wa mafunzo na wakufunzi baada ya mafunzo ya siku tatu mkoani Morogoro.Picha na Michael Mgozi

Kampuni ya Nukta Afrika imetoa mafunzo kwa waandishi wa habari radio za kijamii juu ya namna ya habari za uongo na upotoshaji zinazotolewa na baadhi ya mitandao ya kijamii, hususa ni kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.

Na,Michael Mgozi

Waandishi wa Habari nchini wametakiwa kuhakikisha wanatoa taarifa za kweli na zenye uhakika huku jamii ikiaswa kuwa makini na habari wanazopata kupitia mitandao ya kijamii kwa kujilidhisha kabla ya kuzisambaza.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mafunzo ya siku tatu Mkoani Morogoro, Mkuu wa Mafunzo na utafiti kutoka Kampuni ya Nucta Afrika, Daniel Samson amesema mafunzo hayo yametolewa kwa waandishi wa habari wa Radio za kijamii ili kuwajengea uwezo juu ya kukabiliana na habari za uzushi na uongo na kuwawezesha kuandika habari za kweli kutoka katika vyanzo sahihi.

Sauti ya Mkuu wa Mafunzo na utafiti kutoka Kampuni ya Nucta Afrika, Daniel Samson

Aidha Samson ametoa wito kwa Waandishi kuiepusha jamii na taarifa za uongo, nakuwataka wananchi kuhakikisha wanakuwa makini pindi wanapopata taarifa kutoka katika mitandao, na kutokuzisambaza bila kujilidhisha.

Sauti ya Mkuu wa Mafunzo na utafiti kutoka Kampuni ya Nucta Afrika, Daniel Samson

Kwa upande wao waandishi waliopatiwa mafunzo, wamesema mafunzo hayo yatawasaidia kuandika habari za ukweli na ukakika katika kuuhabarisha umma.

Sauti ya baadhi ya washiriki wa mafunzo

Mafunzo hayo yameandaliwa kwa pamoja kwa kushilikiana  na Kampuni ya Nukta afrika, na Shirika la Internation Media Suport(IMS) kwa ufadhili wa Shirika la maendeleo la Swiden(SIDA) kwa lengo la kuongeza wigo wa kupata taarifa sahihi kwa jamii zitakazosaidia kukuza maendeleo kwa wananchi.