Sengerema FM

Mzee Lugega akabidhi tofari elf.2 ujenzi ofisi ya Ccm,Kwa niaba ya Ngeleja

4 June 2025, 5:37 pm

mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa Mwanza Bi Elizabethi Watson Nyingi akikabidhi mifuko ya cement aliyo ahaidi kwa ajili ya ujenzi ofsi ya Kata Ibisabageni.Picha na Joyce Rollingstone

Aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Sengerema na waziri wa zamani wa nishati na madini Wiliam Mganga Ngeleja ametimiza ahadi yake aliyoitoa kwenye harambee ya ujenzi Ofisi ya Kata ya Ibisabageni ya kutoa Tofari 2,000, zilizo kabidhiwa leo na Ndg.Festo Lugega.

Na;Joyce Rollingstone

Jumla ya tofari   Elfu Mbili na Mia Tano zimetolewa kwa ajiri ya Ujenzi wa Ofisi ya Chama cha Mapinduzi CCM katika kata ya Ibisabageni Mjini Sengerema Mkoani Mwanza.

Ndugu Lugega Festo akikabidhi Tofari elf 2 kwa ajili ya ujenzi ofisi ya CCM kata ya Ibisabageni kwa niaba ya aliyekuwa mbunge wa Sengerema Ndg.Wiliam Mganga Ngeleja.Picha na Joyce Rollingstone

Akikabidhi tofari hizo mwakirishi wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Sengerema Mh Wiliamu Mganga Ngeleja Ndug, Lugega Festo Petro, ikiwa ni kutekeleza ahadi aliyotoa katika halambe ya ujenzi wa ofisi hiyo ya Ccm.

Sauti ya Ndugu Lugega Festo Petro akizungumza baada ya kukabidhi ahadi ya tofari kwa ajili ya ujenzi wa ofsi ya CCM Kata Ibisabageni.

Sambamba na hilo, pia Lugega amewakabidhi tishert 50 wanakikundi cha Wanawake na Samia kilichopo katika kata ya ibisabageni, ikiwa ni kuunga mkono jitiahada za akina mama hao.

Muonekano wa ofsi ya zamani ya CCM kata ya Ibisabageni Mjini Sengerema.Picha na Joyce Rollingstone
Sauti ya Ndugu Lugega Festo Petro akizungumza baada ya kukabidhi ahadi ya shirt kwa kikundi cha mwanamke na Samia kata ya Ibisabageni.

Naye mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa Mwanza Bi Elizabethi Watson Nyingi, amekabidhi mifuko  10 ya Saruji ikiwa ni kutekeleza ahadi aliyoitoa katika halambee ya ujenzi wa ofisi hiyo ,na kusema kuwa amefulahishwa na kuanza kwa ujenzi huo.

Sauti ya mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa Mwanza Bi Elizabethi Watson Nyingi akizungumzia kutekeleza ahadi yake

Katibu wa Ccm kata ya Ibisabageni Bwn, Barnabas Charles Butondo, amewashukuru wote waliotimiza ahadi zao, na kuahidi kutumia tofali na saruji hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa.

Sauti ya Katibu wa Ccm kata ya Ibisabageni Bwn, Barnabas Charles Butondo akishukuru baada ya kupokea ahadi za viongozi kwa ajili ya ujenzi wa Ofsi ya CCM kata ya Ibisabageni

Ujenzi wa ofisi hiyo utarahisisha utoa huduma kwa wanachama wa CCM kwani ofisi iliyokuwa ikitumika awali imechakaa kutokana na kutumika kwa mda mrfeu.

Ndugu Lugega Festo akikabidhi Tshrit kwa kikundi cha Mwanamke na Samia kata ya Ibisabageni kwa niaba ya aliyekuwa mbunge wa Sengerema Ndg.Wiliam Mganga Ngeleja.Picha na Joyce Rollingstone