Sengerema FM

Mtoto wa mwaka mmoja afa maji wilayani Sengerema

3 June 2025, 3:26 pm

Baadhi ya ndugu na majilani wakiwa katika familia ya mtoto aliyefariki kwenye dimbwi la maji kijiji cha Tabaruka wilayani Sengerema.Picha na Emmanuel Twimanye

Kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha kwa baadhi ya maeneo nchini Tanzania, mashimo na madimbwi yamejaa maji jambo linaloweza kusababisha maafa kama watoto watacheza kwenye maeneo hayo,na katika wilaya ya Sengerema mtoto mmoja amefariki baada ya kuzama kwenye dimbwi lililokuwa na maji.

Na,Emmanuel Twimanye

Mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu aliyefahamika kwa jina la Tekela Simon amefariki Dunia baada ya kuzama kwenye dimbwi la maji   katika  kata ya Tabaruka ya zamani Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza.

Wazazi wa mtoto huyo wamesikitishwa na tukio hilo na kueleza kuwa walikwenda shambani na kumwacha mtoto huyo na wenzake nyumbani  na kwamba   baada ya kurudi hawakumkuta ndipo walipoanza kumtafuta na kumkuta amezama kwenye dimbwi la maji na kupoteza maisha .

Sauti za wazazi wa mtoto Tekela Simon aliyekufa maji baada ya kutumbukia kwenye dimbwi

Baadhi ya ndugu na majirani wa familia hiyo wamepokea tukio hilo kwa masikitiko na kuomba wazazi kukufukia madimbwi hatarishi yaliyopo karibu na makazi yao ili kunusuru maisha ya watoto.

Sauti ya baadhi ya ndugu na majilani wa familia hiyo wakizungumzia namna walivyopokea taarifa za tukio hilo

Mwenyekiti wa mkitongoji cha Tabaruka ya Zamani Abdallah Masasila amethibitisha kutokea kwa tukio hilo  na kuwataka wananachi kuwa makini na watoto .

Sauti ya mwenyekiti wa mkitongoji cha Tabaruka ya Zamani Abdallah Masasila akizungumzia tukio hilo

Kwa upande wake Jeshi la  Polisi Wilaya ya Sengerema limefikia eneo la tukio  na kuruhusu ndugu  kufanya taratibu za mazishi.

Baadhi ya ndugu na majilani wakiwa katika familia ya mtoto aliyefariki kwenye dimbwi la maji kijiji cha Tabaruka wilayani Sengerema.Picha na Emmanuel Twimanye.