Sengerema FM

Mwalimu, mchungaji mbaroni kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa miaka 10

21 March 2025, 7:07 am

Mwenyekiti CCM Wilaya ya Sengerema DM akimjulia hali mtoto aliyebakwa alipolazwa katika Hospitali Teule Sengerema. Picha na Emmanuel Twimanye

Matukio ya ubakaji wilayani Sengerema yanazidi kushamiri ambapo taarifa inayozungumzwa ni ya mtoto mwenye umri wa miaka 10 anayedaiwa kubakwa na watu wawili kwa nyakati tofauti.

Na,Emmanuel Twimanye

Jeshi la Polisi Wilayani Sengerema mkoani Mwanza linawashikilia watu wawili   akiwemo mwalimu wa shule ya msingi  Daud  Ochieng (37)  na  Adon Sospeter  (53) wakazi wa kata ya Ibisabageni kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi (10) wa shule ya msingi Bukala wilayani Sengerema kwa nyakati tofauti  .

Akizungumzia tukio hilo mtoto aliyedaiwa kubakwa akiwa amelazwa katika Hospitali teule ya Wilaya ya Sengerema  amekiri kubakwa na watu hao kwa nyakati tofauti .

Sauti ya Mtoto akizungumzia matukio aliyofanyiwa

Mama mzazi wa mtoto huyo amesikitishwa na tukio hilo na kueleza kuwa baada ya kugundua afya ya mtoto wake imedhoofika  ndipo aliamua kumpeleka Hospitalini kwa ajili ya uchunguzi wa kitabibu ambapo uchunguzi huo ulibaini kuwa amebakwa.  

Sauti ya mama mzazi wa mtoto anaye daiwa kubakwa na mwalimu pamoja na mwenye nyumba

Baba mzazi wa mtoto huyo amesema  kuwa taarifa za kubakwa mtoto wake alipata akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake na kumshauri kumpeleka Hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu .

Sauti ya Baba mzazi wa mtoto anaye daiwa kubakwa na mwalimu pamoja na mwenye nyumba

Kufuatia tukio hilo Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi  (CCM)  na Katibu wa umoja wa wanawake (UWT)  Wilayani Sengerema  wamefika katika Hospitali teule ya Wilaya hiyo kumjulia hali mtoto huyo  na kuomba sheria kuchukua mkondo wake dhidi ya watuhumiwa wanaodaiwa kufanya kitendo hicho.

Sauti ya Mwenyekiti CCM na katibu UWT Sengerema

Naye kamanda wa polisi Mkoani Mwanza Wibroad Mtafungwa amethibitisha  kukamatwa kwa watuhumiwa wote wawili  na wapo mahabusu katika kituo cha Polisi Wilayani Sengerema na kwamba watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria mara baada ya uchunguzi wa tukio hilo utakapokamilika .

Sauti ya kamanda wa polisi Mkoani Mwanza Wibroad Mtafungwa akizungumzia matukio ya ubakaji
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mwanza Wibroad Mtafungwa akizungumzia matukio ya ubakaji mkoani Mwanza. Picha Jeshi la polisi Mwanza