Sengerema FM

SEUWASA yakabidhi pikipiki na kutoa onyo kwa atakae bebea abilia

14 March 2025, 7:44 pm

Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya maji Mjini Sengerema Sadala Sadick akikabidhi funguo ya pikipiki kwa watumishi SEUWASA. Picha na Emmanuel Twimanye.

Ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji safi mjini Sengerema Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira (SEUWASA) imekabidhi pikipiki 5 kwa watumishi wa idara ya Ufundi na huduma kwa mteja wa mamlaka hiyo.

Na,Emmanuel Twimanye

Watumishi wa Mamlaka ya maji Mjini Sengerema Mkoani Mwanza  wametakiwa  kutotumia pikipiki walizopewa na serikali  kinyume na matumizi ya mamlaka hiyo ikiwemo Bodaboba na uhalifu .     

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya maji Mjini Sengerema Sadala Sadick wakati akikabidhi pikipiki kwa watumishi wa mamlaka hiyo na kuwataka kutumia pikipiki hizo kwa kazi za mamlaka hiyo na si vinginevyo.

Sauti ya Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya maji Mjini Sengerema Sadala Sadick akitoa maelekezo kwa taumishi baada ya kuwakabidhi pikipiki

Katika hatua nyingine  Mhandisi Sadick  amesema kuwa   hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika maeneo ya mjini ni asilimia  94  huku pembezoni ni asilimia 76 .

Sauti ya Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya maji Mjini Sengerema Sadala Sadick akizunguumzia upatikanaji wa huduma ya maji mjini Sengerema

Nao baadhi ya watumishi wa mamlaka hiyo waliopewa pikipiki hizo wameishukuru serikali kwa kutoa usafiri huo kwa kuwa utarahisisha utendaji wao wa kazi ikiwa ni pamoja na kuwafikia wananachi kwa urahisi tofauti na hapo awali.

Sauti ya baadhi ya watumishi wa Seuwasa wakizungumzia furaha yao baada ya kukabidhiwa pikipiki