Sengerema FM

Waganga wapigwa marufuku kufanya mapenzi na wagonjwa

28 February 2025, 6:46 pm

mwenyekiti wa chama cha waganga na wakunga wa tiba asili mkoani Mwanza Shabani Ramadhani akizungumza wa waganga wilayani Sengerema. Picha na Emmanuel Twimanye

Waganga wa kienyeji wamekua na tabia ya kufanya mapenzi na wagonjwa wao jambo ambalo limepingwa na viongozi wa chama wa CHAWATIATA kuwa nii kosa na si maadili ya kazi hiyo.

Na,Emmanuel Twimanye

Wagaga   wa tiba asili   Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza   wameonywa kuacha mara moja   tabia ya kufanya ngono  na wagonjwa pindi  wanapokwenda kupata huduma za matibabu .    

Onyo hilo  limetolewa na mwenyekiti wa chama cha waganga na wakunga wa tiba asili mkoani Mwanza Shabani Ramadhani katika  kikao cha waganga wa tiba asili kilichofanyika wilayani Sengerema .

Sauti mwenyekiti wa chama cha waganga na wakunga wa tiba asili mkoani Mwanza Shabani Ramadhani

Mwakilishi kutoka ofisi ya mkuu wa upelelezi na makosa ya jinai  wilayani Sengerema  Inspekta   Athumani Waziri amekiri kupokea  malalamiko  ya kulalamikiwa baadhi ya waganga  kufanya ngono na wagonjwa na kuwataka waganga kuachana na vitendo hivyo.

Sauti ya Mwakilishi kutoka ofisi ya mkuu wa upelelezi na makosa ya jinai  wilayani Sengerema  Inspekta   Athumani Waziri

Nao baadhi ya waganga wa tiba asili waliohudhuria kikao hicho wameiomba serikali kuwachukulia hatua kali  za kisheria  waganga watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo  kwa kuwa wanachafua kazi hiyo. 

Sauti ya Wagaanga wwa tiba asili wilayani Sengerema