Sengerema FM

VTC Sengerema yaendelea kuzalisha vijana wenye ujuzi nchini

12 October 2024, 4:39 pm

Picha ya pamoja ya viongozi wa chuo cha ufundi Sengerema VTC na mgeni Rasmi kwenye mahafali chuoni hapo.Picha na Deborah Maisa

Serkali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewekeza fedha nyingi kujenga vyuo vya ufundi nchini ili kukabiliana na changamoto ya uhaba wa ajira kwa vijana, waweze kujiajiri kupitia ufundi.

Na;Deborah Maisa

Wahitimu wa chuo cha ufundi Sengerema vtc wametakiwa kusoma kwa bidii pindi wanapojiandaa  kufanya  mhihani wa kuhitimu elimu ngazi ya chuo

Wito huo umetolewa na mgeni rasmi Mchungaji Adam Malindi kwenye mahafari ya tano tangu kuanzishwa kwa chuo hicho na kuwaeleza wahitimu hao ili waweze kufaulu mitihani yao lazima wazingatie yale waliyofundishwa darasani.

Sauti ya mgeni rasmi Mchungaji Adam Malindi kwenye mahafari Sengerema VTC

Nae mkuu wa chuo cha ufundi Sengerema vtc Yela Aloyce Malando  ameishukuru Serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kwakuanzisha chuo cha ufundi sengerema ambacho kimewawezesha watoto wa kitanzania kujiunga na chuo hicho na kupata ujuzi wa fani mbalimbali.

Sauti ya mkuu wa chuo chaufundi Sengerema vtc Yela Aloyce Malando akiishukuru serkali kwa kuanzisha chuo cha veta Sengerema

Nao baadhi ya  wahitimu wa chuo hicho kwaupande wao wamesema ujuzi walioupata utawawezesha kujiajiri wenyewe na kuajiliwa katika makampuni ndani na nje ya nchi.

Sauti za baadhi ya wahitimu wa chuo cha ufundi Sengerema

Serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa rais Dr. Samia Suluhu Hasan umekuwa ikijenga vyuo vya ufundi veta kila wilaya ili kuhakikisha kila mtoto anapata ujuzi.