Sengerema FM

Moto wazuka na kuteketeza vitu vya ndani mjini Sengerema

6 October 2024, 5:05 pm

Wananchi na gari la zimamoto wakiwa nje ya nyumba ambapo viongozi na baadhi ya wananchi wakiendelea kuzima moto.Picha na Emmanuel Twimanye.

Matukio ya moto kuzuka gafla kwenye nyumba za watu wilayani Sengerema imekuwa ikijitokeza mara kwa mara ambapo jeshi la zimamoto na uokoaji limeendelea kutoa tahadhali kwa wananchi wilayani hapo.

Na;Emmanuel Twimanye

Moto  umezuka  ghafla  na kuteketeza vitu mbambali ikiwemo  magunia ya mpunga  ,  vitanda   na magodoro  katika nyumba ya mkazi mmoja wa mtaa wa Geita Road kata ya Nyatukala    Wilayani Sengerema  Mkoani Mwanza,huku chanzo cha moto huo kikiwa bado hakijafahamika .

Akizungumzia tukio hilo Siwema Helman  ambaye ni  mpangaji wa nyumba hiyo amesema kuwa wakati  wakiwa nje ghafla  walisikia watoto wakipiga kelele na walipokwenda kuangalia kwenye chumba cha watoto waliona moshi huku Godoro likiteketea kwa moto.

Sauti ya Siwema Helman  mpangaji amabye vitu vyake vimeteketea kwa moto ndani.

Baadhi ya wananchi wa  mtaa huo   wamesikitishwa na tukio hilo na kueleza kuwa  baada ya kutokea moto huo  wameshirikiana na Jeshi la zima moto  na uokoaji na kufanikiwa kuzima moto huo  .

Sauti za Baadhi ya Wananchi wakizungumzia tukio hilo
Maguni ya mpunga yalivyoteketea kwa moto ndani.Picha na Emmanuel Twimanye

Mwenyekiti wa mtaa wa Geita Raod Pelana Bagume    amethibitisha  kutokea kwa tukio hilo  na  kuwaomba wananchi kuhakikisha kila mmoja anakuwa na namba za  jeshi la zima moto ili yanapotokea majanga ya moto    wapate  msaada haraka.   

Sauti ya Mwenyekiti wa mtaa wa Geita Raod Pelana Bagume    amethibitisha  kutokea kwa tukio la moto mtaani kwake

Mkuu wa Jeshi la Zima moto  na Uokoaji  Wilayani Sengerema  Juma Ngwembe   amewataka wananchi  kuwa makini na moto ikiwa ni pamoja na kutowaruhusu watoto kuchezea  viberiti ili kuepukana na matukio hayo huku akiwashukuru wananchi waliojitokeza kushiriana na jeshi hilo kuzima moto .

Sauti ya Mkuu wa Jeshi la Zima moto  na Uokoaji  Wilayani Sengerema  Juma Ngwembe akizungumza namna walivyoshirikiana na wananchi kuzima moto
Vitanda vilivyoteketea kwa moto ndani.Picha na Emmanuel Twimanye